Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa muda. Kwanza sina shaka na dhamira na uwezo wa Mheshimiwa Dkt. Tizeba hata kidogo ila nina mashaka na dhamira na focus ya Wizara ya Fedha ambayo asilimia 65 ya Watanzania wanaishi katika sekta ya kilimo, ufugaji na uvuvi lakini development budget tuliyopeleka kwenye kilimo ni asilimia tatu na kwenye mifugo ni asilimia nane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa mkononi ninayo barua aliwahi kuiandika Mheshimiwa Rais Magufuli akimuandikia wakati huo Waziri wa Fedha, Ndugu Mustapha Mkulo mwaka 2009 na nitamkabidhi kaka yangu, nitaomba wahudumu wampelekee Mheshimiwa Waziri. Mheshimiwa Rais Magufuli wakati huo akiwa Waziri wa Mifugo alitaja changamoto saba zinazokabili sekta ndogo ya maziwa katika nchi hii. Mpaka leo zile changamoto ziko hai, unaona ni namna gani Serikalini kuna tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya mifugo kwa maana ya sekta ya ngozi, katika nchi ya Ethopia asilimia 47 ya GDP ya Ethiopia inachangiwa na sekta ya mifugo na sekta ya kahawa. Sisi ni wa pili na ningeomba niweke kumbukumbu sawa humu Bungeni tunasema watatu Sudan imeshagawanyika sasa hivi nchi ya pili Afrika kwa mifugo mingi ni Tanzania. Hata hivyo, hawa wafugaji tunawasaidiaje? Nataka nikupe mifano namna gani Serikali inawafilisi wafugaji wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Ngara katika hii operesheni ya kufukuza wafugaji, zaidi ya ng’ombe 2,047 za wafugaji ambao walinyang’anywa mifugo yao zimefilisiwa leo ni watu maskini. Waziri kwenye kitabu anazungumzia mauzo ya hay, yale majani yale yanayofungwa ya thamani ya Sh.55,000,000. Ukipiga hesabu ni sawasawa na hay 20,000, are we serious? Hay 20,000 ni chakula cha ng’ombe kwenye shamba la mtu mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ilani yetu ya Uchaguzi hii hapa, ukurasa wa 14 na 15 unazungumzia namna gani tutaweza kuongeza uzalishaji wa mifugo bora kwa wafugaji. Ilani yetu ya Uchaguzi imeweka target ya kupeleka mitamba 10,000 kwa wafugaji wetu. Waziri anazungumzia mitamba 500 kwa mwaka, Ilani inazungumzia mitamba 10,000. Mabwawa kwa mwaka katika kipindi cha 2015-2020, Ilani yetu inazungumzia kuchimba mabwawa 2000 mpaka sasa bajeti ya mwaka jana na ya mwaka huu hakuna fedha za mabwawa. How can we help this country? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali, hatuwezi kufikia dhamira ya industrialization kama hatutowekeza kwenye kilimo na ufugaji katika nchi hii. GDP yetu ni Dola bilioni 52, bilioni 15 inatoka katika sekta ya Agro lakini hatuwekezi yaani sekta inayotuingizia bilioni 15 tunapeleka only three percent of our budget. Hii inasikitisha sana na inaenda against our promises kwa wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri akija hapa atueleze, leo tumbaku inaporomoka na ninavyoongea hivi leo gulio la tumbaku limezuiliwa Tabora, ame-project mwenyewe kwamba mwaka huu 2017/2018 yaani Serikali kabisa inapanga kwamba zao la tumbaku litashuka, wana mpango gani kwa hawa wakulima watakaopata umaskini kutokana na zao kushuka na ni namna gani umaskini wao unakuwa compensated kwa mazao mengine, hakuna mpango. Waziri amefanya kazi kubwa ya kufuta tozo ambayo itatusaidia bei yetu kuwa competitive kwenye soko la dunia, jambo jema lakini kama hatuwekezi kwenye production hizo tozo zote anazofuta kaka yangu Mheshimiwa Tizeba hazitakuwa na manufaa yoyote yale kwa wananchi wetu wala uchumi wetu.