Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nianze kwa kuipongeza Wizara kwa hotuba nzuri yenye malengo ya kuinua uchumi wa nchi yetu kupitia kilimo, uvuvi na mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu. Kama tunavyofahamu kilimo kimeajiri takribani asilimia 75 ya wananchi lakini kimeweza kuzalisha chakula almost asilimia 100 ambacho kinatumiwa na wananchi wa nchi yetu hii na
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba sana Mheshimiwa Waziri atusaidie Mkoa wa Katavi hasa Wilaya
kuzalisha malighafi nyingi kwa ajili ya viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yote hayo bado Serikali imeendelea kutenga fedha kidogo kwa ajili ya Wizara hii ya Kilimo tena kinyume kabisa na Azimio la Maputo ambalo linahitaji Serikali kutenga asilimia 10 ya bajeti yake kwa ajili ya kilimo. Ni wakati sasa wa Serikali kuhakikisha kwamba inalifanyia kazi azimio hili kama kweli tunataka kuijenga Tanzania, hatutaweza kuijenga bila kuendeleza sekta hii ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze sasa kuchangia changamoto za masuala ya Wizara hii ndani ya Mkoa wangu wa Mwanza, nitajikita sana katika masuala ya uvuvi. Kumekuwa na malalamiko mengi kwa miaka mingi kutoka kwa wavuvi ambao wanavua katika Ziwa Victoria na wapo baadhi ya wenzangu ambao tayari wameshatangulia wameliongelea hili lakini jinsi lilivyo nyeti suala hili na mimi nitaendelea kuliongelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama wote mnavyofahamu kuwa mimi ni mwakilishi wa vijana, tena ninayetokana na Mkoa wa Mwanza, ambapo vijana wengi wamejiajiri na kuajiriwa katika sekta ya uvuvi. Hata pale ambapo kunatokea na migomo mbalimbali ya uvuvi lazima vijana hawa wanaathirika kwa namna moja au nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, uvuvi katika Ziwa Viktoria una manufaa makubwa kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa na Taifa kwa ujumla kwa sababu kuna mlolongo wa wafanyabiashara wengi ambao wananufaika kutokana na uvuvi huo. Wapo akinamama ambao wanakaanga na kuuza samaki katika vijiwe mbalimbali; wapo ambao vijana ambao wameajiriwa katika viwanda vya samaki na katika mialo ya samaki; wapo wafanyabishara wanaosafirisha samaki ndani na nje ya nchi; wapo watu ambao kazi yao ni kusafisha tu samaki hawa; wapo wafanyabiashara pia ambao wamenufaika kwa namna mbalimbali kutokana na uvuvi huu wa Ziwa Viktoria na pia wapo mamilioni ya Watanzania wanaotegemea kupata kitoweo kutoka katika ziwa hilo na kupata virutubisho kwa ajili ya kujenga afya yao. Hao ni baadhi tu ya wanufaika wa uvuvi wa Ziwa Viktoria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, unapotengeneza mazingira magumu kwa mvuvi wa Ziwa Viktoria ujue ni namna gani unavyoathiri uchumi wa nchi. Wavuvi hawa hawa wamekuwa wakishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuwabaini wale ambao wanavua kwa njia haramu. Hivyo basi wana haki ya kusikilizwa mahitaji yao kwa sababu yamekuwa ni ya muda mrefu na naamini kabisa pale Serikali itakapoamua inaweza kuyatatua matatizo haya na yakafika mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wavuvi hawa mara nyingi wamekuwa wakiomba kuruhusiwa kuuza samaki tofauti na bondo. Mabondo yamekuwa ni gharama kuliko hata mnofu wa sangara. Leo hii mvuvi analazimika kuuza samaki pamoja na bondo lake ina maana yule anayenunua ndiyo ananufaika zaidi, wakati wao ndio wanaotoa jasho. Niombe Serikali iweze kuliangalia suala hili, nafahamu ina wataalam wengi ambao wanaweza wakakaa wakamshauri Waziri pamoja na Naibu wake wapate kuliangalia hili na namna gani wavuvi hawa wanaweza kunufaika kutokana na hayo mabondo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mara nyingi wamekuwa wakiomba kuondolewa vikwazo vya kuuza samaki mbichi mzima katika masoko ya nje ya nchi. Wapo wavuvi wakubwa na wadogo, lakini wapo wale ambao wanaweza kusindikika na kupaki, ifike wakati sasa Serikali ione...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.