Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naomba niipongeze Serikali kwa namna ya pekee ambavyo imekuwa ikitenda kazi na kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi katika Jimbo la Nsimbo 97% ni wakulima, 3% ni watumishi ambao ni kada upande wa walimu na huduma ya afya. Kwa maana hii ni kwamba, Wilaya hii inagusa sana Jimbo la Nsimbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Nsimbo 55% ya mapato ya ndani yanatokana na zao la Tumbaku, lakini tumekuwa na changamoto na nimshukuru Waziri kuna tozo amezipunguza hapa, lakini katika hizi tozo kumi, tozo nne zinagusa wakulima, tozo sita zinagusa makampuni.

Sasa Mheshimiwa Waziri, hizi tozo zinazogusa makampuni kwa tani 60,000 ambazo haya makampuni wanatarajia kununua, ukichukua average cost per ton na hiki alichokipunguza is very minor. Hai-promote katika wakulima kupata bei nzuri kwa haya makampuni kununua Tumbaku; kutoka 4,000 mpaka 2,000 na hizi 4,000 nyingine alizofuta. Kwa hiyo, nakuomba Mheshimiwa Waziri uliangalie tena, libakie la wakulima, la makampuni liondoke kwa sababu hai-promote kwenye bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, wakati wa Mkutano wa Wadau wa Tumbaku, Morogoro, mwaka 2016 Desemba, Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba suala la bei na kuna sheria ambazo zitakuja, tutaweza kuzibadilisha hapa ndani. Sasa tutaomba wakati wa majumuisho atuambie ni lini zinakuja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kumekuwa na malalamiko sana kwa upande wa wakulima kuhusiana na ukaguzi unaofanywa na COASCO. Hii COASCO iangaliwe, kwa sababu ukiangalia tija yao katika ukaguzi wa vitabu vya mahesabu vya vyama vya msingi bado kuna mahali wanapita wanatoa Hati Safi lakini badaye unakuta kuna ufujaji wa pesa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri angalia WETCU Tabora. Waziri Mkuu kafanya ziara, ameibua, kasimamisha watendaji na Bodi, lakini rudi nyuma kwenye ripoti za COASCO. Kwa hiyo, COASCO iangaliwe kama uongozi ubadilishwe, mfumo na utendaji wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoangalia zao la Tumbaku tuangalie na mazingira. Ni zao ambalo linahitaji sana miti. Mmetoa mabanio kidogo ya kisasa, lakini pia makampuni yanaenda yanashusha kiwango cha kununua. Ukiangalia katika hotuba ya Waziri, mwaka wa fedha 2015/2016 kwa tumbaku ni 60,691 na takwimu hiyo hiyo ikaenda 2016/2017, lakini 2017/2018 itakuwa 55,900. Kwa hiyo, kiwango kinashuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa watu masikini ambao ni wakulima waliozoea kulima tumbaku, wanahitaji zao mbadala. Kwa nini tunahitaji zao mbadala? Tayari nchi imeamua kuwa ya viwanda. Tatizo kwenye tumbaku limeshaonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaiomba Wizara, ile mapping ya mazao nchi nzima kwa kila Wilaya yanastawi mazao gani? Tuweze kugawiwa tuwape wananchi wetu wapate mazao mbadala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona tuna demand ya viwanda. General Tyre sasa hivi raw materials anatoa wapi? Bakhresa anatengeneza juice, raw materials nyingi inatoka nje ya nchi, kwa nini yasitoke humu humu? Kuna maeneo mengine watu hawana uelewa kwamba hapa ninaweza nikalima zao gani kwa sababu tangu mkoloni mtu amezaliwa, tangu mababu analima mazao hayo na watu wanaendelea hivyo hivyo. Kwa hiyo, Wizara kwa kupitia Halmashauri zetu, itoe hizo takwimu na sisi wanasiasa, Wabunge na Madiwani tusaidie kuelimisha wananchi. Hii itasaidia viwanda vipya vinavyokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna viwanda vya zamani vinavyohitaji raw materials na wengi wananunua kutoka nje na matokeo yake pesa nyingi ya kigeni tunazitumia kuagiza malighafi kwa ajili ya viwanda badala ya kwamba tuwekeze kwenye kilimo zaidi, tupunguze pesa ya kigeni kwenda nje ili balance of payment iendelee kuwa positive na ndiyo uchumi ambavyo unaenda unakua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna suala limezungumziwa hapa na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge, kuhusu utafiti, mambo ya research, nami niungane mkono nao. Mwaka 2016 tumepitisha hapa Bungeni The Tanzania Agriculture Research Institute Act, 2016 na tumepitisha The Tanzania Fishers Research Institute Act, 2016. Kuna Bodi zinatakiwa ziundwe kwenye hizi institutes, je, mpaka sasa hivi zimekwishaundwa na kazi zimeanza? Kwa sababu inawezekana zile nyadhifa za Rais bado hajakumbushwa kuweza kuteua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Waziri utatupa mrejesho wa hizi sheria mbili tulizopitisha na hizi Bodi kama zimeanza kazi na faida yake ni ipi? Kwa sababu tunajua, moja ya majukumu ya Bodi kama Agriculture Research Institute, ni kuishauri Serikali katika national policies, laws na regulations mbalimbali kwenye mambo ya Kilimo. Sasa badala ya kukaa tunalalamika hapa mambo ya research na sheria tumeshatunga, ni suala ambapo mnatakiwa Wizara sasa ndiyo mkimbie badala ya kutembea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna suala la pembejeo. Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini mvua zinawahi kuanzia mwezi wa kumi. Serikali ijaribu kuangalia kwamba pembejeo hizi zije kwa wakati, na pia ruzuku iwepo. Serikali imekuwa na jitihada kubwa sana tangu Uhuru. Nilikuwa naangalia Hansard swali la mwaka 1963 liloulizwa na Marehemu Philipo Mbogo, kwamba ni lini Serikali italeta matrekta na majibu ya Serikali, ilikuwa kwamba kwa kupitia Agriculture Credit Agency watapeleka matrekta Mpanda by that time.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mikakati hii tangu baada ya Uhuru ya kunyanyua kilimo, tukaja Benki ya CRDB hatukuifanyia vizuri, matokeo yake Benki ya CRDB imekuwa benki ya kibiashara badala ya kusadia vyama vya ushirika na wakulima. Sasa hivi tuna Tanzania Agriculture Development Bank. Mtaji ni mdogo, wakulima wetu kule kwenye vyama vya msingi wanakopa kwenye benki ya biashara, wanatozwa riba kubwa, lakini benki mahususi ambayo imeanzishwa kwa ajili ya kilimo, bado haiwasaidii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malengo, kama ilivyokufa CRDB imekuwa benki ya kibiashara isije na hii Benki ya Maendeleo ya Kilimo na yenyewe ikaangukia vile. Kuna uwiano kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara, kuna ile kitu inaitwa MUVI (Muunganisho wa Ujasiriamali Vijijini). Wakulima wanafundishwa, wanapewa mbegu bora, Kwa Nsimbo lini watakuja? Mawasiliano kati ya Wizara ya Viwanda na Kilimo yako wapi?

Pia katika tafiti tuangalie, tunaenda kwenye nchi ya viwanda, kuna writeup ya Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli wakati akichukua Doctorate alifanya writeup kwa kuangalia utomvu kwenye mabibo ya korosho jinsi gani yanaweza kutumika katika kuondoa kutu. Kwa hiyo, ni moja ya vitu ambavyo tunaweza tukaviangalia na vikatusaidia katika nchi yetu kuweze kuendeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie kuhusu umwagiliaji. Tunaishi kwa kudra za Mwenyenzi Mungu, tunategemea mvua. Mikoa kati hapa mwaka huu imekosa mvua. Sisi kule tumebahatika, kwa nini tusiende kwenye umwagiliaji? Tunatumia maji kwa ajili ya kunywa. Maji ya Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Mto Malagarasi. Kwa nini tusiende kwenye kilimo cha umwagiliaji? Tunavyoleta maji huku kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya domestic, kwa nini tusitengeneze na mabwawa yakatumika kwa umwagiliaji? Nile inalisha huko Ethiopia na Misri.