Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia katika Wizara hii ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uzima, hatimaye kuwawakilisha wananchi hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuwapongeza Mawaziri wote kwa uchapakazi wao mzuri na uwajibikaji. Hakika hawa Mawaziri hawajakaa maofisini kama tunavyojua Maofisa wanavyokaa maofisini kusubiri changamoto. Wamekuwa wakizunguka Mikoa kwa Mikoa, Majimbo kwa Majimbo kuhakikisha wanajua changamoto za wananchi. Mheshimiwa Rais hakukosea kuwateua, hakika Mungu awasaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii pia kumpongeza Waziri wa Kilimo na Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri wanazozifanya. Pamoja na changamoto wanazozipata za hali ya hewa, lakini wamekuwa wakichapa kazi kuhakikisha wanaendeleza Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi ya pekee kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa uchapakazi wake mzuri, kwa uwajibikaji, hatimaye kuliletea Taifa nidhamu. Rais huyu amekuwa akifanya kazi usiku na mchana japokuwa kuna watu wamekuwa wakimbeza wakisema Rais huyu ni wa ajabu, siyo kweli!

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais huyu ametenda maajabu ambayo hawakuyategemea. Rais huyu kwa muda mfupi tu ameweza kufanya mambo makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ameweza kuhakikisha kwamba watoto wanasoma bure, pili, ametengeneza barabara zote, sasa hivi zinapitika kwa kiwango cha lami, tatu, ameweza kununua ndege, mmeziona, mmeshuhudia na nyingine bado zinakuja, Rais huyu amefanya mambo mengi sana. Amerekebisha mambo mengi sana! Ni mtambo wa kurekebisha tabia za mafisadi! Mungu amjalie huko aliko, nasi tupo nyuma yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijielekeze sasa kwenye suala la pembejeo. Mkoa wa Rukwa umekuwa ni mkoa ambao unalima mazao mengi yanayokubali. Mkoa huu umekuwa ulikilisha mikoa mingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi iangalie mikoa hii ambayo mvua ni za uhakika ipeleke pembejeo kwa wakati. Huu mpango ambao umeanza kutumia mawakala, naomba mawakala wapeleke pembejeo kwa wakati hatimaye wananchi wa mikoa hii wapate kulima kilimo kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la Benki ya Kilimo. Benki hii tunaisikia Dar es Salaam na Arusha. Nilikuwa naiomba Serikali, kwa sababu kuna mikoa ambayo mvua ni za uhakika na kilimo ni cha uhakika, ipelekwe benki hii ianzishe mabenki mikoa yote, ikiwezekana wilaya zote, wakulima waweze kukopa pesa za kulima na kukopa matrekta, itasaidia sana kuongeza kiwango cha kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la Soko la Samaki la Kimataifa. Mkoa wa Rukwa, Wilaya ya Kalambo lilianzishwa Soko la Samaki la Kimataifa, lakini mpaka sasa hivi soko hili linaonekana kama limetelekezwa. Kule Kalambo Ziwani kunapatikana samaki wengi sana ambao ni migebuka, sangara na samaki wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo inaonekana kwamba kwa sababu ya kukosa lile soko, kwamba halifanyi kazi, wanakuja Wakongo na Wazambia wanavua samaki mle tani na tani, wanapeleka huko. Serikali na Halmashauri zinashindwa kupata mapato na wananchi pia hawapati mapato, hilo soko haliwasaidii. Naomba Serikali ilifufue hilo Soko la Samaki la Kimataifa ili wananchi waweze kufaidiaka na Serikali pia iweze kufaidika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo machache, naunga mkono hoja. Ahsante sana.