Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Riziki Saidi Lulida

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nimshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema ambaye amenijalia kuwepo leo na kuweza kuchangia katika hoja hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimshukuru Mwenyezi Mungu amjalie Maalim Seif Sharif Hamad kipenzi cha Watanzania hasa Wazanzibar ambao walijitahidi kumpatia kura za ndiyo lakini Mwenyezi Mungu anasema walatazidu-dhwalimiina ila hasara. Imetendeka hasara kubwa na dhuluma kubwa lakini mwenye kuwa na kiburi duniani hapa ni Mwenyezi Mungu peke yake alaysallah bi-ahkami-l-haqimiina. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nataka nizungumzie suala la ajira. Uchumi wa Tanzania umechukuliwa na wageni, wageni wameuchukua uchumi wetu kwa kupitia ajira za Tanzania. Sasa hivi ukiingia katika viwanda vyetu ambavyo viko katika Manispaa wafanyakazi walioko mle ndani wengi ni wageni na wametengeneza maukuta mtu yeyote hata mfanyakazi anayetoka Wizara ya Kazi hawezi kuingia mle. Maana yake ni kuwa uchumi ukipelekwa kwa wageni Watanzania watabakia kuwa ni maskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitatoa mfano, Dangote ameanzisha kiwanda Mtwara lakini mpaka sasa hivi wamegundulika wafanyakazi 360 kutoka nje ambao hawana vibali. Kwa maana hiyo, wananchi au Watanzania ambao wanahitaji kupata kazi pale hawana nafasi lakini nafasi hizo zimechukuliwa hasa na sura pana. Tujiulize, hawa sura pana ndani ya nchi hii wamekuwa kama panya ndani ya ghala, wanakula karanga wanatubakishia maganda na nitaitolea ufafanuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri zetu hasa za Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ambazo tunalima korosho sasa hivi sura pana wanakwenda kununua mazao ndani ya vijiji. Huu ni uhuru ambao hauna mipaka. Kule vijijini wanakokwenda wanafanya kazi nyingi sana. Kwanza, wanasema wananunua korosho, ufuta lakini kazi kubwa wanayoifanya kule ni uwindaji haramu. Sasa hivi tunaona misitu imekwisha, tembo wamekwisha, tujiulize wako hapa kutusaidia au wamekuja kutuharibia uchumi wa nchi yetu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini napata kigugumizi sana, tunaona watu wanawasifia, jamani hatujioni kama tunateketea? Tuko katika uchumi mgumu tunahakikisha kila kinachopatikana kinakwenda kwa wageni. Tufike mahali tujiulize tutakaa lini tujitambue, tuache uzembe ili tuangalie hawa sura pana wapo kutusaidia au wamekuja hapa kutumalizia uchumi wetu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitazungumzia suala la zao ya korosho katika Mikoa ya Kusini. Tuna export levy zinapatikana zaidi ya bilioni 30, hizi pesa hazijulikani zinakwenda wapi. Tulitegemea hizi pesa zikafanye kazi ya kutengeneza madawati, kununua dawa, ni ulaji ambao hauna mipaka ndani ya mikoa hiyo. Naomba tusimamie hela za export levy tuzijue zinakwenda wapi maana zimeliwa kwa miaka mingi mpaka sasa hivi haijulikani kinachoendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Mkoa wa Mtwara wana export levy, katika hela hizo 60% zinakwenda kwa Mkuu wa Mkoa anazitumia kwa kitu gani? Hakuna madawati, dawa…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Lulida nilikupa dakika tano na zimekwisha.