Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia bajeti hii muhimu sana ambayo inabeba asilimia 65 ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Dkt. Tizeba na Naibu Waziri, Mheshimiwa Olenasha kwa kazi nzuri wanayoifanya kusimamia hizi Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Pia nichukue nafasi hii kupongeza Kamati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, kwa kweli wamefanya kazi nzuri ya uchambuzi wa sekta hizi muhimu kwa Watanzania na nina imani kwamba Serikali itazingatia yale mapendekezo mazuri ambayo Kamati imetoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina machache ya kuchangia katika bajeti hii, naomba nianze na suala la kodi kero 17 ambazo zimeondolewa. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kutimiza ahadi ambayo aliahidi wakati wa uchaguzi na kodi kero hizi ziko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Mheshimiwa Rais tunakupongeza sana na tunakuombea ili uendelee kuchapa kazi tutimize zile ahadi ambazo tuliwaahidi Watanzania katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada hizi nzuri, changamoto bado zipo, kwa sababu nia ya Serikali katika kuondoa kero hizi 17 kwenye kahawa ili kumsaidia mkulima wa kahawa bei ya kahawa iweze kupanda. Kuondoa kodi ni hatua muhimu katika kupandisha bei, lakini bei ni factor ya zaidi ya kodi, kuna thamani ya bidhaa yenyewe. Sasa ili zao la kahawa liweze kupanda bei sambamba na upunguzwaji wa hizi kodi kero, Wizara inawajibika kuwasaidia wakulima wa kahawa kuongeza thamani kwenye ile bidhaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa kuna Mfuko wa Kahawa ambao baadhi ya kodi zilikuwa zinaenda kwenye ule Mfuko ili uweze kumsaidia mkulima wa kahawa aweze kulima kahawa ambayo ina thamani. Mfuko huu sijui unasimamiwaje, umekaa kimya, nimefuatilia naambiwa Mfuko hauna hata shilingi moja. Naomba Wizara irudi kuhakikisha Mfuko huu wa Kahawa zile kodi zilizotakiwa ziingie katika Mfuko huu ili uweze kumsaidia mkulima wa kahawa, basi tumsaidie mkulima wa kahawa ili kahawa anayolima iwe na ubora. Kwa vile Serikali imeshaondoa kodi kero hizi 17, basi kahawa ikiwa na ubora ukaongeza hizi kodi ambazo zimetolewa, zitamsaidia mkulima wa kahawa kupata bei nzuri katika kahawa hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kodi hizi ambazo zimeondolewa nyingi zimelenga kwenye zile kampuni ambazo zinasindika, sasa trickle down effect ya kodi lazima Serikali isimamie kuhakikisha hii reduction ya kodi ambayo imetolewa inaenda kwa mkulima kwa sababu ndiyo nia ya Serikali kumsaidia mkulima wa kahawa. Kwa hiyo, kupitia Bodi ya Kahawa, kupitia Vyama vya Ushirika Serikali iendelee kufanya hizi reforms ili tuone mwisho wa siku mkulima wa kahawa ndiye anayenufaika along the value chain.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika hili, napenda kuiomba sana Wizara, mara nyingi tunaziachia Halmashauri ndizo zihangaike na kumsaidia mkulima wa kahawa, lakini suala la miche, kama nilivyosema ule Mfuko wa Kahawa, wekeni fedha za kutosha ili tuwasaidie wakulima wapande kahawa kwa wingi na kwa sababu sasa hivi tumeshawaondolea kodi kero ili uzalishaji upande.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata Serikali sasa hivi hizi kodi kero ambazo zimeondolewa, ina maana imekosa mapato kwa upande mmoja, lakini tukimsaidia mkulima wa kahawa akapandisha uzalishaji kilimo cha kahawa Serikali itapata mapato kupitia Kodi ya Mapato na halmashauri pia kupitia zile tozo ambazo wanatoza na wenyewe mapato yatapanda. Kwa hiyo Serikali itakuwa imepoteza kwa upande mmoja lakini ime-gain kwa upande mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende katika mchango wa kilimo kwenye Pato la Taifa. Naomba nitaje takwimu chache ili kuonesha picha ya hali ya Sekta ya Kilimo katika kuchangia Pato la Taifa. Nakumbuka sekta hii ndiyo inayogusa asilimia 65 ya Watanzania, kwa hiyo ni muhimu sana hizi takwimu zikai-alarm Serikali kwamba tujitahidi tufanye reform ambayo itapelekea jitihada nzuri ya Serikali ya kuweka miundombinu ili kutupeleka kwenye uchumi wa kati, jitihada nzuri za Serikali kuhakikisha tunakuwa na uchumi wa viwanda. Ili tuweze kuwa na hiyo socio-economic transformation ya kubeba asilimia kubwa ya Watanzania lazima takwimu hizi tusifanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya kilimo kwa miaka sasa imegota kwenye asilimia 28 mpaka 29 kama mchango kwenye pato la Taifa. Hii inatuambia kwamba tukiweza ku- double ukuaji wa sekta ya kilimo kwenye pato la Taifa tutakuwa tumewasaidia Watanzania asilimia 65. Kwa hiyo, tuna kila haja ya kuhakikisha tunaisaidia hii Wizara ipate fedha za kutosha kufanya miradi ya maendeleo ili iweze kuinua asilimia kubwa ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia sekta hii inakua kwa asilimia 1.7 takwimu za 2016, mwaka 2005 sekta hii ilikuwa inakua kwa asilimia 5.2, unaona trend inarudi chini, ni lazima Serikali ifanye kila jitihada ili tuweze kurudisha hii trend ianze kupanda, kwa sababu kukua kwa sekta hii ndiko kunamsaidia Mtanzania ajikwamue kutoka kwenye umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni sehemu ya Azimio la Maputo, hata Kamati ya Kilimo na Mifugo wamelitaja hili. Mwaka 2016 bajeti ya Serikali asilimia 4.9 tu ndiyo ilienda kwenye Sekta ya Kilimo; mwaka 2010 ilikuwa ni 7.8, kwa hiyo unaona trend nayo inashuka. Kwa hiyo, naomba sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Kamati ya Bajeti, kaeni tuangalie hizi takwimu zinatupeleka wapi, lazima tuzi-reverse hizi trends tuanze kuelekea kwenye kuhakikisha asilimia 10 ya bajeti ya nchi inaenda kwenye sekta ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia disbursement ambayo inaenda kwenye sekta ya kilimo, haiendi yote. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri na Kamati, kilimo peke yake disbursement ilikuwa ni asilimia 3.3, hii ni kidogo mno. Naiomba Serikali kabla ya mwezi Juni kwisha jitahidini angalau tuende kwenye asilimia 50 mwezi ujao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata kwenye mifugo kiasi kilichoenda ni asilimia nane tu, hizi takwimu ni alarm, inabidi tufanye u-turn ili tuweze kwenda kwenye trend nzuri ambayo itawainua asilimia kubwa ya Watanzania. Kwa kufanya hivyo, tutahakikisha miundombinu ambayo Serikali ya Awamu ya Tano inaijenga kukuza uchumi inasaidia Watanzania walio wengi. Kwa kufanya hivyo, tutaweza kutengeneza malighafi ambazo zitaenda kwenye viwanda hivi ambavyo tunataka kuvitengeneza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hoja hiyo ya mchango wa kilimo kwenye Pato la Taifa, sasa niende kuipongeza Serikali kwa kuleta utaratibu wa Fertilizer Bulk Procurement. Utaratibu huu ni mzuri sana, naipongeza Serikali kwa sababu inaonesha dhamira yake kutaka kumsaidia mkulima aweze kupata mbolea. Katika hili, pamoja na hii jitihada nzuri, Serikali zote duniani huwa kwenye planning na coordination kwa sababu Serikali ni kubwa… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.