Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kabla sijaanza kuchangia Wizara hii, naomba niungane na mchangiaji mmoja aliyetangulia, anaitwa Profesa Jay. Mheshimiwa Waziri naomba nimpe ushauri kidogo, kabla sijaendelea kuchangia, anapokuja kwenye Majimbo yetua jaribu kutushirikisha Wabunge wenye Majimbo.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwambia hili kwa sababu mimi huwa sitaki nikae na kinyongo na huwa sitaki tufanye kazi kwa kinyongo na Waziri wangu. Alikuja Jimboni kwangu, ameenda kufanya mkutano na wananchi, anawaambia wananchi Mbunge wenu yuko wapi? Ameanza kuruka sarakasi kama za Bungeni? Mheshimiwa Waziri hii haifai hata kidogo na kwa wananchi wangu hii siyo haki hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amefanya hivi pia kule kwa Profesa Jay na Majimbo mengine. Alikuja Mheshimiwa Mwigulu Nchemba Jimboni kwangu, ameniandikia message, amenipigia simu nimempa ushirikiano mzuri. Kwa hiyo, naomba wakati mwingine ajaribu kuwa na ushirikiano na mahusiano mazuri na Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba ukuaji wa Sekta ya Kilimo umeendelea kushuka mwaka hadi mwaka. Ukuaji wa Sekta ya Kilimo, tunaambiwa kwamba ni asilimia 1.7 kwa takwimu za NBS na hii unakuja kuona sasa hata bajeti ambayo imetengwa kuanzia mwaka 2010/2011 tuliona asilimia 7.8 ambayo ndiyo ilikuwa bajeti kubwa kwa mara ya mwisho. Tumekuja kuona mwaka 2011/2012, ikawa asilimia 6.9 mwaka jana, 2016/2017 ni asilimia 4.9.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kuwasaidia wakulima wa Tanzania kwa kuendelea kutenga bajeti ya kilimo kidogo kiasi hiki. Naomba niseme tu kwamba Maputo Declaration walipendekeza kwamba angalau nchi wanachama wa AU wajaribu angalau kutenga asilimia 10 kwenye bajeti za kilimo. Hii Maputo Declaration kwa Tanzania tutakuja kuitekeleza lini? Kwa hiyo, naomba niseme kwamba ili kuwasaidia Watanzania hebu tujaribu kutenga bajeti ya kutosha. Kwa mazingira haya, hatuwezi kupata viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, jana nimemwona ndugu yangu hapo Waziri wa Viwanda amebeba makabrasha mengi sana, lakini kwa bajeti hii ya kilimo, kwa kweli naamini kabisa hata Waziri wa Viwanda asitegemee kuwa na viwanda kwa sababu hawezi kuwa na viwanda bila kuboresha kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, historia inatuonesha duniani popote pale, walifanya mapinduzi kwenye kilimo. Tunajua ile Agrarian Revolution iliyofanyika kule Britain, tunajua Agrarian Revolution iliyofanyika kule Marekani, tunajua Indian Green Revolution, tunajua ile China Green Revolution ndipo tukaona sasa wenzetu viwanda vinakuja. Viwanda ni matokeo ya kuboresha kilimo na kupeleka fedha nyingi na kuhakikisha kwamba wakulima mambo yao yanakwenda vizuri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano viwanda vya nguo, wanategemea pamba; bila kuwekeza kwenye pamba hatuwezi kuwa na viwanda. Bila kuwekeza kwenye mbegu kwa mfano kama alizeti na ufuta hatuwezi kuwa na viwanda vya mafuta. Kwa hiyo, niseme tu kwamba Mheshimiwa Waziri naomba tafadhali, ajaribu kushauri. Najua tu tatizo la viongozi wetu walio wengi hasa Mawaziri mnamwogopa Bwana mkubwa. Hii ndiyo shida kubwa! Mwambieni ukweli, msiogope! Ukweli ndiyo utakaokuweka huru. Kwa bajeti hii, hatuwezi kufika popote na mwakani tutarudi kuja kupiga kelele tena hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna jambo ambalo Mheshimiwa Waziri amezungumza kwenye hotuba yake kuhusu suala la bulk procurement ya mbolea. Siyo jambo baya, lakini naomba tungekuwa tuna-focus zaidi kwenda kujenga viwanda vya mbolea nchini kote.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukijenga viwanda kwa mfano ukajenga Kiwanda cha Mbolea kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambao ni wazalishaji wakubwa sana, ukijenga kiwanda kwa mfano Kanda ya Kaskazini, ukajenga Kiwanda cha Mbolea Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kati, Mheshimiwa Waziri mbolea itashuka bei. Kwa sababu tunajua kabisa, kwa mfano, hili suala la saruji, leo kidogo bei ni nafuu kwa sababu viwanda vya saruji viko vingi. Watafanya biashara ya ushindani na mwisho wa siku mbolea itashuka bei. Kwa hiyo bulk procurement ni jambo moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, hili la kujenga viwanda. Tungeendelea kabisa kufikiria hili zaidi kuliko tukawa na hizi kuzibaziba tu angalau kwa muda mfupi, haliwezi kutusaidia sana. Kwa hiyo, naomba niseme tu kwamba alikuja hapa Mfalme wa Morocco, Mohamed wa Sita, tukamwomba atujengee uwanja wa mpira Dodoma. Nadhani wanapokuja watu wetu, kama hawa wadau wa maendeleo, tungekuwa tunawaomba wawekeze kwenye viwanda vya mbolea. Wakiwekeza kwenye viwanda vya mbolea, wakulima wetu watanufaika. Mbolea itashuka bei.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo nchi yetu zaidi ya miaka 50 baada ya uhuru tunamwomba mtu uwanja wa mpira badala ya kumwomba viwanda vya mbolea! Mheshimiwa Waziri kwa kweli mimi hili naona siyo sahihi kabisa. Naona leo tumeomba viwanja vya mpira, kesho tutaomba jezi, kesho kutwa tutaomba mipira. Hili jambo halitatufikisha popote pale. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa niweze kuzungumzia jambo lingine kwenye bei ya zao la kahawa. Zao la kahawa limeendelea kushuka bei miaka yote. Wenzetu wa korosho mmerekebisha mambo vizuri kabisa kule, leo korosho wananufaika kweli kule Kusini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kahawa imeendelea kushuka bei mwaka hadi mwaka. Ndugu zetu wa jirani tu hapa wa Kenya wanauza kahawa bei nzuri, Uganda wanauza kwa bei nzuri, Tanzania ni nani aliyeturoga? Tatizo liko wapi, Tanzania kahawa yetu tunauza kwa bei ndogo? Leo wakulima wangu Mbozi kule wameamua kuanza kung’oa miche ya kahawa kwa sababu wameona hailipi. Wanaamua walime mazao mengine kwa sababu ya bei ndogo ya kahawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuwasaidie wakulima hawa wa Kahawa, tupandishe bei na ikiwezekana kabisa tuweze kuangalia namna gani ya kuweza kupandisha bei. Kwa nini tusiende kujifunza kwa majirani zetu? Mbona Kenya siyo mbali, hata kwa pikipiki unafika hapa jirani Kenya! Mbona Uganda siyo mbali, kwa nini tusiende kuwauliza ninyi mnauzaje kahawa yenu kwa bei nzuri? Kwa nini Tanzania sisi hatuuzi kahawa yetu kwa bei nzuri?

Mheshimiwa Waziri kwenda kujifunza kwa ndugu yako siyo dhambi hata kidogo! Naomba sasa tukajifunze tuangalie wenzetu, kwa nini wanauza kahawa yao kwa bei nzuri, tuone sisi tuliteleza wapi, tuweze kuwasaidia wakulima wa kahawa, zao ambalo linaelekea kwenda kufa siku za hivi karibuni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, naomba nizungumzie suala la kuanzisha Mnada wa Kahawa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Leo nchi nzima, Watanzania wanaolima kahawa wanaenda Moshi kwenye Mnada wa Kahawa. Tukianzisha Mnada wa Kahawa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, kwa mfano, tukaweka Kiwanda cha Kahawa pale Songwe au tukaweka Mbeya, wakulima wetu wataenda kushiriki moja kwa moja kwenye Mnada wa Kahawa pale. (Makofi)