Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru sana kunipa nafasi hii ya kipekee ili nichangie Wizara hii. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Tizeba kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Wizara yake nzima kwa sababu kwa kuanzia nimeona kwa kweli mnafanya kazi. Kuna mambo ambayo tumewaomba siku si nyingi sana lakini mmeshayarekebisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kama mvuvi; mimi nimetokea kwenye dagaa dagaa kwa hiyo mimi pia ni mvuvi; nimeona hapa kuna baadhi ya tozo tulizokuwa tunazilalamikia. Kwa mfano kuna hii tozo ya movement permit, kuna hizi ada za ukaguzi wa kina wa viwanda na maghala zimepunguzwa, vilevile kuna tozo za vyeti vya afya ambayo ilikuwa inawasambua sana wavuvi hawa. Pamoja na hayo vile vile pia kuna ada za usajili wa vyombo vya uvuvi ambayo ni kati ya vitu ambavyo Mheshimiwa Tizeba na Wizara yake wamevishughulikia, kwa kweli pongezi sana nakupa na Mungu awabariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kipekee bado niendelee kuomba baadhi ya vitu ili waviangalie, pia vipate punguzo kwa ajili ya kuwasaidia wavuvi hawa au hawa wafanyabiashara wa samaki. Kwa mfano sasa hivi ushuru umeongezwa ambapo gunia moja kutoka shilingi 1000 kwenda shilingi 2000, kitendo kinachowapelekea wale wafanyabiashara kukosa faida ambayo wangeitegemea na faida yao ni kidogo sana. Kwa hiyo, wanapotozwa tozo kubwa inasababisha faida zao kupungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kipekee nimuombe sana Mheshimiwa Tizeba, Mkoa wetu wa Mara ni Mkoa uliozungukwa na Ziwa Victoria, lakini ni kati ya mikoa ambayo mara kwa mara huwa tunakuwa na upungufu wa chakula. Nimuombe Mheshimiwa Tizeba ashughulikie suala hili kwa kushughulikia kilimo cha irrigation, kwa maana ya kwamba tuwe na kilimo cha kudumu mkoani kwetu ili sasa tuepukane na hili suala la shida ya chakula cha mara kwa mara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee suala ambalo limezungumziwa jana na Mbunge mwenzangu wa Jimbo la Serengeti, Mheshimiwa Ryoba, kwa kweli Mkoa wa Mara kumekuwa na upungufu wa chakula na ni hali ambayo ipo nchi nzima na dunia nzima ya mabadiliko ya hali ya hali ya hewa. Lakini Mbunge mwenzangu aliongela kwamba chakula sasa hivi hakuna kabisa kwa sababu ya tembo. Mimi nimwambie Mheshimiwa Ryoba, Serikali sikivu, Serikali ya Mheshimiwa Magufuli imeshapeleka chakula mpaka sasa tani 500 na mimi nilimuomba Mheshimiwa Tizeba ambaye aliomba chakula Ofisi ya Waziri Mkuu na wamela na wataleta katika Mikoa mingine yote walioomba. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Ryoba kwa kuwa yeye ni Mbunge wa Serengeti, mimi ni Mbunge wa Mkoa kwa hiyo kuna taarifa nyingine anapaswa kuniambia mimi ili niwe nampa kwa sababu ameshindwa kusimamia wananchi wake na mimi ndiye nasimamia mambo hayo na nimeomba na wameshaleta chakula. (Makofi)

Lakini kutokana na hili suala la tembo, ni kweli linasumbua lakini wanakuja kwa msimu, sio wanakuja siku zote, tembo huwa wanakuja wakati mvua hazinyeshi, yaani wakati wa kiangazi.

T A A R I F A . . .

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei hiyo taarifa kwa sababu Mheshimiwa anaongopa mbele ya Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, chakula kimeletwa tangu juzi na ripoti ipo, lakini yeye ameomba Mwongozo siku ya jana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ryoba nikuombe unishukuru kwa kazi ninayokufanyia jimboni kwako. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna hili suala la tembo. Ni kweli suala sumbufu kwa Wilaya ya Serengeti na Wialaya zingine. Hawa tembo huwa wanakuja wakati wa kiangazi, wakati mvua zikinyesha hakuna tembo anayekuja kutafuta maji kwa sababu huwa wanakuwa wana maji. Hata hivyo Serikali yetu sikivu imelishughulikia pia suala hili na inaendelea kulishughulikia, na mimi niliongozana na Mheshimiwa Ramo Makani, Naibu Waziri kwa ajili ya kufanya mipango jinsi ya kuziba au kuzuia yale maeneo ili hawa tembo wasiwasumbue wananchi. Nafikiri Mheshimiwa siku hiyo sijui alikuwa na mawazo mengi, lakini tulikuwa naye, sijui kama alisahau. (Makofi)

Mheshimwia Naibu Spika, kwa hiyo mimi nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge mwenzangu kwamba tukae na tuongee na wananchi wetu, tuwaombe lakini pia tuwaeleweshe kwa sababu ukweli ni kwamba sisi tunapokaa yale maeneo ni maeneo ambayo yamepakana na hifadhi, ambako zile ndizo njia za tembo, kwa mfano, kuna Robanda, Manchila, Kisangula, Sedeko, Mbalibai, Mashoswe, Nata, Mosongo, Nyamatale, Uwanja wa Ndege (maeneo ya Ngalawani), haya yote ni maeneo ya ukanda wa hifadhi. Ki ukweli ni kwamba yale maeneo tunayokaa sisi ni kweli tunaathirika lakini ni maeneo ambayo sisi ndo tumewafuata wale tembo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi niwaombe ndugu zangu Wana-Serengeti, kwa hali hii tuvumilie katika kipindi hiki ambacho Serikali yetu inalishughulikia suala hili, na nina imani kabisa ni suala ambalo litaisha na haya matatizo yote yataisha. Hata hivyo tusiwape imani wananchi wote kwamba eti njaa inaletwa na tembo, kuna maeneo mengine ambayo tembo hawafiki, je, huyu Mheshimiwa ambako tembo hawafiki anawapeleka yeye?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna mambo ambayo tunapaswa sisi kuyaongelea kama Wabunge, lakini kuna mambo ambayo hatupaswi kuyalalamikia na kulia kwa muda wote. Tukiwa tunalia sisi wananchi wetu watafanya nini? Tunapaswa sisi tuongee na Serikali yetu kwa lugha ya kuwaonesha au kuwaelekeza kwamba kuna matatizo kwa sababu sisi ndio tunaishi kule, isiwe tu tunakuja tunasema kwamba ooh kuna hiki kuna hiki, kibaya zaidi tunaenda kufanya kule siasa. Wananchi sasa hivi hawataki siasa wanataka vitendo.

Mheshimiwa Mbunge mwenzangu, basi mimi na wewe tujipange, kile chakula kimeshaletwa, twende tukawagawie wananchi wetu kusudi waepukane na hili tatizo lililokuwepo kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoongea mabaya na mema pia tuongee. Kuhusu hili hili suala la tembo, kuna fidia ambazo zimeshalipwa na Serikali, sijamsikia Mheshimiwa Mbunge mwenzangu hapa anaisifia Serikali, na bado kuna pesa nyingine ambazo Mheshimiwa Rais ameandaa zitakazokuja kwa awamu nyingine ya pili. Kwa hiyo, wanasema mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Serikali yetu ni sikivu, Serikali yetu ina nia njema…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.