Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kuangalia kilimo na elimu kuwa kipaumbele cha kwanza ili viwanda vyetu viweze kupata malighafi kutoka kwa wakulima wetu ili kukuza uchumi wa kaya. Nishauri Serikali kupitia sera zake za viwanda kuzihuisha ili ziendane na wakati wa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, nashauri Serikali itunge sheria na adhabu kali zinazotokana na uharibifu wa mazingira, hasa utiririshaji maji ya viwandani ambayo yamekuwa kero kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kurejesha viwanda vyote vilivyobinafsishwa kutumika kinyume na mkataba wa awali. Mfano, Kiwanda cha Korosho Kibaha kimegeuzwa mahali pa kutunzia bidhaa, hivyo matumizi yaliyoainishwa wakati wa mkataba kukiukwa. Naishauri Serikali kupunguza urasimu katika kusajili biashara na kupelekea wawekezaji kushindwa kuwekeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu viwanda na wanawake, naishauri Serikali kuwaangalia kwa jicho la huruma wasaidiwe ili kuweza kupata mikopo ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo. Mfano, viwanda vya vyakula vya kuku na mashine za kutotolea vifaranga ili waweze kujikwamua kiuchumi.