Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, natoa pongezi kwa hotuba nzuri yenye kusheheni mambo mazuri na taarifa kwa umma. MUVI, imefanya wilaya na mikoa saba tu hivyo basi ni muhimu kuongeza wilaya nyingine na hasa Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mpanda katika Halmashauri ya Nsimbo.

Mheshimiwa Naibu Spika, NEDF. Mfuko huu bado haujasaidia wajasiriamali kwa kuwa bajeti ni ndogo hivyo Serikali itoe kipaumbele kwa kuongeza mtaji ili wananchi wakope.

Mheshimiwa Naibu Spika, Maafisa Biashara katika Halmashauri. Bado hatujaona jinsi Maafisa Biashara katika Halmashauri wanavyotumika kuendeleza kazi za Wizara katika Halmashauri zetu, hivyo basi Sekretarieti ya Mkoa inafaa kupewa majukumu ya kuendeleza masuala ya viwanda katika mkoa.