Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja. Bidhaa zinazoingizwa bila kukidhi viwango.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kushauri kuwa vifaa vinavyokamatwa kutoka nchi za nje kama mabati ambayo tatizo lake ni Specfication, yaani geji isiyokuwa sahihi badala ya kuviharibu vitiwe chapa ya bei kulingana na hali yake halisi ili vitumike kwa shughuli nyingine kama kujengea mabanda ya mifugo kuwekea fensi pia ujenzi wa nyumba za muda mfupi. Kuviharibu ni kupunguza level ya uchumi na vina impact kwenye GDP kwani kuna fedha zimetumika toka kwa wazawa (domestic).

Mheshimiwa Naibu Spika, bei za bidhaa kuwa juu (bidhaa za viwanda vyetu). Wizara hii ishirikiane na Wizara ya Fedha kulinda bei ya bidhaa inayotengenezwa ndani; kuweka VAT kwenye bidhaa inayoanza kuzalishwa nchini na kupandisha bidhaa hiyo kwa walaji wa ndani kwa kuwa inamvutia mzalishaji kuuza nje ya nchi kwa ajili ya zero rated concept ya export zote. Pia kupoteza ushindani kwa bidhaa inayozalishwa au kuingizwa kutoka nje hususani nje kwenye upatikanaji wa material ya bei rahisi, technology ya hali ya juu na sera zao juu ya exports zao. Nashauri VAT itazamwe vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda vya pembejeo. Nashauri Wizara iweke mkazo sana kwenye viwanda vitakavyozalisha pembejeo, yaani mbolea, madawa pamoja na vifaa vya kilimo. Pia maduka ya vifaa vya kilimo yawekwe maeneo ya wakulima sambamba na mafunzo kwa wananchi ili wajue au wapate elimu ya umuhimu wa kutumia vifaa vya kisasa kuwawezesha kuwa na kilimo chenye Tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.