Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa anayofanya katika Wizara hii muhimu lakini anaifanya peke yake bila hata kuwa na Naibu Waziri wa kumsaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuonesha malalamiko yangu juu ya kukosekana kwa soko la uhakika la zao la ufuta. Namwomba Mheshimiwa Waziri aliangalie suala hili ili tupate soko la uhakika la zao la ufuta, wakulima waweze kupata fedha stahiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu suala la kuwezesha wakulima wa chumvi kupata uwezeshaji wa kupata mkopo wa mashine ya kusindika chumvi ili kuinuna kipato chao. Naomba Mheshimiwa Waziri aweze kuwaunganisha wakulima hao wa chumvi na SIDO ili SIDO iwapatie mashine hizo hata kwa mkopo ili tuweze kufungua kiwanda cha kusindika chumvi hivyo wakulima hao waweze kujiongezea kipato zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutambua miaka michache iliyopita kulikuwa na taarifa ya uwepo wa Kiwanda cha Simenti pale Mchinga. Taarifa za kiwanda hicho zilikuwepo tangu wakati Jimbo la Mchinga linaongozwa na Mheshimiwa Mudhihir Mohamed Mudhihir lakini hadi sasa hatuna taarifa zozote kutoka katika mamlaka husika. Tunaomba kujulishwa kiwanda hiki kimefikia wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kuhusu hatua ya viwanda vya LNG. Tunasikia kuwa kuna watu wanataka kuhujumu jambo hili, je, taarifa hizi ni kweli au la?

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu viwanda vya korosho ambavyo vimebinafsishwa lakini watu waliovichukua wanavigeuza kuwa ni maghala tu badala ya kuvitumia kwa ajili ya kuongeza thamani ya korosho kwa kuzibangua. Mheshimiwa Waziri tunaomba wale wote waliochukua viwanda vyetu vya mtama, Nachingwea, Newala na kadhalika wanyang’anywe na viwanda hivyo wapewe watu ambao watavitumia kwa lengo lililokusudiwa.