Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu na msimamo wa Wizara katika yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Wizara itasaidia upatikanaji wa Kiwanda cha Matunda Wilaya ya Muheza; kwa kuwa wafanyabiashara na wakulima wa Wilaya Muheza hawanufaiki na zao la matunda hasa machungwa? Katika Wilaya ya Tanga Mjini Kata ya Kiomoni, kuna Kampuni inaitwa NEEL KHANT Lime Limited Tanga, kinachomilikiwa na Bwana Rashidi Liemba.

Kiwanda hiki kimekuwa na madhara makubwa kwa wakazi wanaozunguka eneo hilo hasa wanafunzi wa Shule ya Msingi na Sekondari Kiomoni. Wizara inafahamu changamoto hiyo? Iko tayari kushirikiana na NEMC kufuatilia usalama wa raia wa eneo hilo?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini Tanga Special Economic Zone (SEZ) imetengewa fedha kidogo; shilingi bilioni
2.7 katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa mwaka 2016/2017 - 2020/2021 wakati Tanga ni Mkoa wa Viwanda? Katika historia ya nchi, Tanga ndiyo mkoa wa kwanza ndani ya nchi hii kuwa na viwanda vingi miaka ya 1980.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwanamke na viwanda. Sensa ya Viwanda inaonesha asilimia 99.5 ni viwanda vidogo sana na viwanda vidogo. Kwa takwimu hizi, ni wazi viwanda vingi vidogo vinamilikiwa na wanawake. Je, Wizara imejipangaje kuhamasisha wanawake kujiunga katika Sekta hii ya Viwanda?

Je, Serikali kupitia Wizara ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa viwanda vinakuwa gender sensitive katika product na ajira?