Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi hii. Pia namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uzima na afya njema. Kabla ya yote, napenda tu pia kumpa pole Mwenyekiti wangu wa Kanda, Mbunge wa Tarime Vijijini, Mheshimiwa John Heche kwa kuumwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine pia napenda nisemee kitu kidogo, imesemewa hoja yake iliyotolewa hapa asubuhi; ni mbaya sana kumsema mtu ambaye anaumwa, yuko hoi kitandani. Ni vizuri mkamwacha akapona ndiyo aje aambiwe hayo maneno anayoambiwa ili ayajibu yeye mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niseme tu kwamba Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mheshimiwa Mbunge hajakataa kiwanda kisijengwe Tarime, isipokuwa utaratibu ufuatwe unavyotakiwa na mwende mkawashirikishe wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda tu kuishauri Serikali kwamba Wizara ya Viwanda na Biashara ni vizuri ikaungana ikawa pamoja na Wizara ya Kilimo, kwa sababu bila kuwa na Wizara ya Kilimo, viwanda haviwezi kufanya kazi zozote kwa sababu wanaendesha viwanda kwa kutoa malighafi wapi? Maana malighafi inatoka kwa wakulima. Kwa maana hiyo basi, ni vizuri hizi Wizara zikaungana ili yale mazao yanayopatikana kutoka kwa wakulima yaende yakafanye kazi katika viwanda. Maana huwezi kusema mnafanya kazi katika viwanda kwa kutegemea mazao ya wakulima halafu Wizara yenyewe inajitegemea yenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano, viwanda vya mafuta; huwezi kuchenjua mafuta bila kutoka kwenye vitu kama karanga, mbegu za pamba, ufuta au alizeti. Kwa hiyo, basi ni vizuri hizi Wizara mbili zikaungana. Kwa mfano, katika Mkoa wa Mara tulikuwa na viwanda vingi sana, karibu viwanda kumi na kitu, lakini sasa hivi ni viwanda vitatu tu vinavyofanya kazi; na ni viwanda vya watu binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namshauri Waziri wa Viwanda na Biashara kwa nini asivifufue vile viwanda vya Mkoa wa Mara? Kwa mfano, kile Kiwanda cha MUTEX, kile kiwanda kilikuwa kinasaidia kutoa ajira nyingi sana kwa wakazi wa Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimshauri tu Mheshimiwa Waziri na Mkoa wa Mara una sifa kuu kubwa moja ambapo ametokea Baba wa Taifa. Ili kumuenzi Baba wa Taifa ni vizuri ikaonekana kwamba kuna kitu ambacho kinaleta manufaa kwa wananchi wake katika Mkoa wa Mara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini atavifufua vile viwanda vya Mkoa wa Mara? Maana tulikuwa na Kiwanda cha Mara Oil ambacho sasa hivi hakifanyi kazi; kuna Mugango Ginnery, tuna Jarif Ginnery, ORAM Ginnery; hivi vingine vilikuwa vya watu binafsi na Buramba Ginnery, vyote hivi havifanyi kazi.

Pia tulikuwa na viwanda vya samaki; na hivi viwanda vya samaki, sasa hivi kinachofanya kazi ni kiwanda kimoja tu ambacho ni cha Musoma Fish. Sasa Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu kwamba wale wavuvi wanapovua samaki, kwa nini wasiwe wanapeleka kwenye kiwanda kuchenjua minofu ya samaki ambayo inasafirishwa kupelekwa nje ili wasilete usumbufu wowote, wawe wanachambulia pale pale Mkoani Mara?

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine kikubwa, ni lazima iwepo mikakati ya Wizara hizi mbili ili izingatie namna ya kumsaidia mkulima pamoja na kuweza kuwasaidia vijana wetu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)