Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Kwanza kabisa naomba sana niipongeze Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi chini ya Rais John Pombe Magufuli kwa kuendelea kutimiza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi kuwa tunajenga Tanzania ya viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa nikiongea kila siku hapa kuhusu Kiwanda cha General Tyre cha Arusha nimeona kimetengewa pesa ili kianze, lakini ninachoomba je, tumejipangaje kuhusu viwanda vingine vinavyotengeneza matairi hasa vya nje? Je, Kiwanda cha General Tyre tumejipangaje ili kifanye biashara vizuri? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nilikuwa naomba reli ya Tanga – Arusha mpaka Moshi. Reli hii itasaidia sana katika usafirishaji wa matairi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Arusha kuna viwanda vingi tu, kuna Kiwanda cha Lodhia Plastic. Kiwanda hiki kimeajiri Watanzania 700; ni kiwanda cha mabomba na ma-sim tank. Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja tulitembelea kiwanda hiki, ni kiwanda chenye ubora wa hali ya juu na aliagiza baadhi ya ofisi zetu za Serikali zitumie kiwanda hiki, lakini ma-engineer wa Serikali wamekuwa wakikwamisha kiwanda hiki. Wamekuwa wakiagiza mabomba nje ya Arusha, wamekuwa wakiagiza mabomba Dar es Salaam ambapo kwanza ni gharama kubwa sana, wamekuwa wakiagiza wakandarasi wanunue mabomba kwenye viwanda fulani, sijui kuna nini (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hizo figisu figisu hizo nahisi kuna rushwa. Tumekuwa tunakwamisha Watanzania ambao wanajitokeza kuendeleza viwanda vyao kutimiza kauli ya Rais wetu Tanzania yenye viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba sana Mheshimiwa Waziri aangalie hili, Mheshimiwa Waziri Mkuu alishatoa amri sijui kama kuna amri nyingine zaidi ya Waziri Mkuu. Tujue hawa ma-engineer wa Serikali ni kitu gani hasa wanapata mpaka wanatoa amri kwa makandarasi ili waende wakachukue mabomba kutoka kwenye viwanda vya nje ya Arusha, kwa sababu kwanza ni gharama. Tunasema tunabana matumizi matumizi gani tunabana kama ni hivi? Tunahujumu na tunamhujumu Rais wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Arusha tuna Kiwanda cha Gypsum kinaitwa Saint Gabain Lodhia Gypsum. Kiwanda hiki kinatumia makaa ya mawe wanatoa Kiwira, mpaka wafike Arusha wanatumia dola 120 mpaka 130. Kiwanda hiki kimekuwa kinatozwa pesa nyingi tofauti na viwanda vingine. Wamekuwa wananunua makaa ya mawe dola 65 mpaka 70; huku viwanda vingine vimekuwa vinatoa dola 35.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamwomba Waziri aangalie sana, tunazidi kukwamisha jitihada za Rais wetu za kuwainua Watanzania. Pia kiwanda hiki kimeajiri Watanzania 450. Hiki cha plastic tayari Watanzania 250 wameshapunguzwa kwa ajili ya hawa watu ambao wanatuhujumu. Ninaomba sana kwa kweli Mheshimiwa Waziri mimi nitashika shilingi nisipopata jibu la kiwanda hiki cha plastic, nisipopata jibu kiwanda hiki ambacho kinatumia Makaa ya Mawe ya Kiwira. Naomba Mheshimiwa Waziri uje na majibu yanayoeleweka ama sivyo sitakuelewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri Mkuu alikuja tulitembelea Kiwanda kimoja cha Hans Paul. Yule ni Mtanzania ana kiwanda, anachukua magari Anaya-design yanakuwa magari ya kubebea taka. Magari yake anauza shilingi milioni 200 mpaka 220. Mheshimiwa Waziri Mkuu mwenyewe aliona alishaanga sana hakutegemea kama watanzania wanaweza wakawa na ujuzi kama huo. Ni magari mazuri na yana ubora wa hali ya juu. Ningeshauri baadhi ya Halmashauri zetu zitembelee zione kuliko uangize magari kwa bei zaidi ya shilingi milioni 500 huku tunaweza tukapata magari yenye ubora wa juu hapa hapa nchini kwa shilingi milioni 220. Naomba sana tulinde viwanda vya ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Arusha tulikuwa na kiwanda kikubwa sana cha dawa kimefungwa mpaka leo na kimefungwa na Tanzania tuna uhaba wa dawa. Kwa nini kisifunguliwe hata kisaidie hata Kanda ya Kaskazini yote?

Naomba sana Mheshimiwa Waziri uje kunijibu na hili kiwanda cha dawa cha Arusha kimefungwa mpaka leo. Naomba sana kiwanda hiki kifunguliwe Serikali ijipange ifungue kiwanda hiki. Tunayosema Tanzania yenye viwanda haitakuwa yenye viwanda bila kutekeleza haya ninayokuambia Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunajua kuna watu ambao walipewa viwanda vilivyokuwa vya Serikali, lakini viwanda vile wameng’oa mashine, viwanda vingi tu havitumiki tena. Tunaomba viwanda hivi mkiweza mvirudishe Serikalini ili vifanye kazi, Watanzania waweze kupata ajira tuweze kutumia na sisi bidhaa zetu. Watu wengi walipwa viwanda lakini wamefanya ma-godown.

Mheshimiwa Naibu Spika, Arusha tunajua ni mkoa ambao unaongoza sana kwa mifugo, ni Mkoa ambao una wafugaji wengi sana. Tunaomba na sisi mtuwekee angalu kiwanda cha ngozi ili tuweze kutumia mifugo yetu na itufaidishe tuweze kutengeza viatu. Ngozi inatengeza vitu vingi sana tunaombasana mtuangalie Arusha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na malalamiko makubwa sana kwa wafanyabiashara, wanakata tamaa wanashindwa kuendelea, tunakwamisha jitihada za Watanzania. Kuna process ndefu sana katika kupata vibali cha kuanzisha biashara. Wanapitia sehemu nyingi sana mpaka wanakata tamaa. Tunaomba sana Mheshimiwa Waziri wasaidie Watanzania wengi, hiki ni kilio cha watu wengi sana. Tunakuomba Mheshimiwa Waziri narudia tena.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba sana mimi leo kweli nitashika shilingi Mheshimiwa Waziri asiponijibu kuhusu Kiwanda cha Plastiki cha Lodhia. Vilevile nilikuwa naomba washirikiane na Waziri wa Maji hata idara zetu za maji mfano kama AUWSA watumie watu ambao wako kwenye mikoa yao maana viwanda ni vizuri, kuna hujuma hapa; na hawa ma-engineer wa Manispaa wa mikoa yetu nilitaka nifahamu wenyewe wana nguvu gani kuliko Mheshimiwa Waziri Mkuu? Kama Mheshimiwa Waziri Mkuu anatoa amri hawaitekelezi wanatuma mabomba wakachukue mabomba Dar es Salaam inawezekana kweli? Wanapatanini? Kwanza gharama ni kubwa; tunasema Serikali yetu tunabana matumizi naomba tusimuangushe Mheshimiwa Rais ana nia nzuri na Watanzania ana nia nzuri na nchi yetu, ana nia nzuri na chama chake ambacho ndiyo anatekeleza Ilani yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, sina mengi, naunga mkono hoja, lakini Mheshimiwa Waziri nitashika shilingi leo.