Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nitumie fursa hii kumpongeza kwa dhati kabisa Mheshimiwa Rais kwa ku- revive dream ya kuwa na industries katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 1967 Mwalimu Nyerere aliasisi dhana ya kuwa na viwanda, na focus ikawa import substitution industries, viwanda ambavyo baadaye vilikuja kufa. Kwenye bajeti ya mwaka jana nilimuahidi kaka yangu Mwijage, kwamba tutakutana na nilionesha mashaka yangu juu ya utekelezaji wa dhamira ya yeye kufikia yale ambayo alikuwa ametarajia, na leo tunayaona.

Mheshimiwa Naibu Spika, vision ya Rais ni kujenga uchumi wa viwanda ambao utalijenga Taifa hili kujitegemea, hii ndiyo vision ya Rais. Kwenye battle field, Chief of Staff na Generals wanachora vita kwenye meza, wanaoenda kupiganisha vita hii ni makamanda. Tuna tatizo kubwa la ku-link vision ya Rais na mikakati yetu ya kuweza kufikia malengo aliyokuwa nayo Mheshimiwa Rais ya kuwa na viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nitoe mifano michache, kwa taarifa ya BOT ya mwezi Aprili, manufacturing industry imeshuka kutoka 1.4 million US Dollar mpaka 817 million US Dollar, maana yake tumepoteza dola milioni 500. Re-Export ime-drop kwa dola milioni 80, fish and fish products ime-drop kwa dola milioni 20, lakini on the other hand credits kwenye agro sector zime-drop mpaka kufika negative 9.2, transport and communication zime-drop by negative 21.6, building by negative 3, hotel and restaurant ime-drop by 7%. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, export of traditional crops, bidhaa pekee iliyo-grow ni korosho na not because of volume, because of price. Tobacco imeshuka kutoka mwaka 2015, three hundred and forty three million US Dollar mpaka milioni 281 mwaka 2017 Machi. Cotton imeshuka kwa dola milioni 10, kahawa imeshuka kwa dola milioni tisa, karafuu imeshuka kwa dola milioni 13. Sisal ime-grow only for one million US Dollar. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, capital goods, capital equipments. Capital goods zimeshuka mpaka negative 16.7, transport imeshuka kwa 23.9, building 19.3, machinery 11.3, what is the problem? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, problem ni un-predictability ya sera zetu za kodi. Nitatoa mfano wa Sheria ya Uwekezaji, kifungu namba 19. Sheria hii tumeibadilisha mwaka 2009 kwa kufuta utaratibu wa deemed capital goods, ikashusha investiment. Tukaibadilisha mwaka 2010;tukaibadilisha mwaka 2012; tunafuta na kurudisha, tukaibadilisha 2014 na tumeibadilisha mwaka 2015. This is the same country sheria ile ile, leo unweka incentive kesho unafuta. Mheshimiwa Mwijage hata ahubiri kwa Injili na Qurani, we will never go through. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nichukue mfano, success ya industrialization ni private sector na Mheshimiwa Rais amesema. Nimechukua kitabu cha miaka mitano cha mpango, hakuna hata page moja inayoongelea namna gani private sector itakuwa included kwenye growth of economy of this country. The problem is a Ministry of Finance that is our biggest problem. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nikupe mfano mwingine, ninayo Ripoti ya World Bank iliyoifanya Tanzania Micro Reform for Agri-Business. Ili uanzishe kiwanda kidogo cha kuzalisha maziwa unatakiwa uwe na documents zifuatazo, upate Incorporation Business Licence kutoka BRELA, Premise Registration, Equipment and Truck Registration, Product Testing and Registration, Staff Health Certificate, On Going Inspection, Import Permit/Export Permit, Weigh Measures; ili uzipate hizi zinatakiwa zipite BRELA, TFDA, TBS, Diary Board, OSHA, Ministry of Labour, Weigh and Measure, NEMC, all of these! Nani anakuja kuwekeza hapa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu, Deputy Managing Director of International Monitory Fund alikuwepo Tanzania, amesifia sana uchumi wetu kwa kipindi cha miaka 20, lakini amesema mambo matatu na naomba ninukuu:-

“(i) It is essential to increase investiment in an effective way to address key bottlenecks in the economy and create more jobs.”

Mheshimiwa Naibu Spika, our area to create jobs ni ku-link industrialization na agriculture, tusipofanya namna hiyo hatuwezi ku-create kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe mfano wa Wamachinga, na nimeongea na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI ameahidi kuipitia hii Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa. Leo tuna Sheria ya Fedha tuliyoifanyia mabadiliko mwaka 2012 ambayo inamtaka mfanyabiashara alipe service levy ya 0.3 percent. Wewe ukiwa unauza coca cola, double taxation angalia hii. Cocacola Kwanza atalipa service levy kutokana na turn over na muuzaji wa Nzega anatakiwa alipe
0.3 on the same product ambayo mmei-tax from the producer mnakuja kum-tax from the agent na mnakuja kum-tax retail seller. How can we grow business like this? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kaka yangu Mheshimiwa Mwijage, utazunguka all over the world. Nataka niwape mfano kuhusu leather industry, waliongea Waheshimiwa Wabunge hapa. Kuzalisha one square feet ya ngozi Tanzania ni senti 14 dola, Ethiopia ni senti 8, India ni senti 7, Pakistan ni senti 8, how can we compete? Na why, kwa sababu, sisi tumeweka export duty ukizalisha ngozi Tanzania kui-export unalipia kodi, uki-import chemicals kwa ajili ya ku-process ngozi unalipa 25% tax, unalipa 18% VAT, how can we grow? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima kabisa nataka niiombe Serikali na Mheshimiwa Waziri wa Fedha, there is no where in the World una-tax inputs. Kodi zote lazima ziwekwe kwenye output, una-tax vipi inputs! Unaongeza cost of production, nani atawekeza? BOT imefanya mabadiliko kwenye mfumo wake wa interest, nani ataenda kukopa? There is no way! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana ripoti ya BOT inaonesha lending imeendelea kushuka kwa sababu hakuna sehemu ya kwenda kufanya biashara. Sasa hivi wanachinga tunakusanya kodi za Halmashauri vibaya mno, hawakui hawa watu, mkulima kodi, mmachinga kodi akianza kufanya biashara yake, mwekezaji kodi. Nataka niishauri Serikali, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda toa direction dunia ijue.

Mheshimiwa Naibu Spika, umefanyika Mkutano wa IFC juzi, one week ago, kujadili emerging economies and where to put money kwenye private sector, Tanzania inakuwa discussed ni area ambayo ni unpredictable. Leo mna sheria hii kesho akija Waziri huyu anabadilisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, there is no way kama Wizara ya Fedha haitaelewa kwamba kodi ni secondary, number one is creation of wealth and creation of job.