Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Kujenga Taifa kazi yake kuu ni kulinda usalama wa Taifa, wananchi na mipaka yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majukumu makubwa ya Wizara hii bajeti hii bado haitoshi ili tuendelee kuwa na amani na utulivu tulionao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya mipaka na Jeshi, Jeshi likiwa imara na wananchi wanakuwa salama katika Taifa. Ni lini Serikali kupitia Wizara hii itatatua mgogoro uliopo katika Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda na Jeshi kuchukua eneo ambalo wananchi wamejenga? Ni lini Serikali itatatua mgogoro huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi liliwakuta wananchi likaazima eneo hili, leo hii linadai eneo ni la Jeshi na wananchi wamekatazwa kujenga na kulima katika eneo hili.

Je, Serikali haioni kwamba Jeshi linataka kuwapora wananchi maeneo yao na mashamba, nani atawalipa fidia wananchi hawa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kiusalama kuweka vifaa vya usalama vya kijeshi karibu na makazi ya watu yaliyopo katika Kata ya Mpanda Hoteli, Misunkumilo, Milala na Makanyagio; je, hamuoni huku ni kuhatarisha usalama kama ulivyotokea mlipuko wa mabomu Mbagala? Naomba majibu kuhusiana na suluhisho hili ili wananchi waondokane na unyanyasaji huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wanajeshi kuboreshewa maslahi yao kama mshahara, pensheni na nyumba zao; kuchelewesha maslahi yao haya kunapelekea baadhi yao kujihusisha na matukio ya ujambazi na uhalifu katika Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matukio ya uhalifu wa watu kuuawa, mauaji ya Kibiti, nini tamko la Serikali ili kuondoa na kumaliza uhalifu huu unaofanywa na baadhi ya wastaafu wanajeshi ambao siyo waaminifu. Ni aibu kuona nguo/vazi la Jeshi kutumika katika matukio ya aibu, Watanzania wana imani na Jeshi hili lakini kwa baadhi ya matukio ya kijinga yanayofanywa na baadhi ya watu yanalichafua Jeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Paulo Makonda, alipoenda kuvamia Clouds Radio alikuwa na watu au wanajeshi wawili waliovaa vazi la Jeshi kwa hili lililotokea hamuoni kwamba imelichafua Jeshi hili, nini tamko la Wizara na Serikali ili kumwajibisha huyu Bashite katika tukio hili, hamuoni kwa Jeshi kukaa kimya linaonesha Jeshi linahusika kufanya haya matukio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi wa mipaka na wananchi katika maeneo yanayopakana na nchi jirani je, mkakati gani unatumika pamoja na kuwashirikisha wananchi elimu kwa raia namna ya kutoa taarifa kuhusu ulinzi na usalama wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Jeshi hili lijikite zaidi katika kulinda usalama wa Taifa na lisitumiwe na watu wenye nia mbaya kwa raia. Maonyesho ya makomando hadharani hamuoni kwamba inawapa mwanya watu waovu kujua ubora na udhaifu wa Jeshi letu. Mazoezi ya Jeshi hadharani yenye tija na sio ya kutisha wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho Jeshi la Kujenga Taifa lisitumike vibaya na utawala wa CCM kwa maslahi ya Chama Tawala, bali Jeshi hili liangalie maslahi mapana ya Taifa.