Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kuimarisha Jeshi la Kujenga Taifa ili liweze kuwa na tija kama miaka ya zamani lilipojenga uchumi badala ya kuwa consumer wa Pato la Taifa. Miaka hiyo Mlale ilitoa mahindi mengi, Mafinga pia, Ruvu ilikuwa wazalisha mpunga na ufugaji ambao ulileta faida kwa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kuweka uwazi katika ajira zinazotolewa ili kuondoa minong’ono iliyopo ya kuwa rushwa inatolewa ili vijana wetu kupata ajira bila usumbufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, nashauri Kiwanda cha Nyumbu kifufuliwe ili watendaji walioajiriwa kwa ajili ya kiwanda wasiligharimu Taifa bila kazi yoyote. Serikali iweze kuona kiwanda hiki kilikuwa na uwezo wa kuongeza ajira na Pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kwamba Vituo vya Jeshi viwekwe mbali na mazingira ya wananchi ili kutoleta migongano na mazoea yaliyopitiliza kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nashauri Serikali iwapatie posho na vitendea kazi askari wetu ili kufanya kazi zao kwa urahisi zaidi.

Vilevile naishauri Serikali kulipa madeni kwa Jeshi linayodaiwa kwa kuwapa fedha zile zilizopitishwa na Bunge badala ya kusitishwa huduma muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali itoe ushawishi wa Watanzania kutumia bidhaa zao ili kuweza kuwaongezea pato.