Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Naipongeza Wizara kupitia wanajeshi wetu kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuilinda nchi yetu na kubaki katika hali ya utulivu na amani. Hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vijana wanaojiunga na JKT mara wamalizapo mafunzo ya kujitolea (kujitegemea), baadhi yao huajiriwa na vikosi vyetu vya ulinzi, lakini baadhi hurudi katika maeneo yetu na kuzurura bila kazi maalum ya kufanya. Je, Serikali haioni sasa wakati umefika kwa vijana hawa wanaopitia JKT kuwa na mfuko maalum wa kuwasaidia vijana hawa mara tu wamalizapo mafunzo, kupewa na kuanzisha miradi na kujiajiri wenyewe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile wakati wakiwa JKT wapewe mafunzo ya ujasiriamali ili wakitoka wawe tayari kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii.