Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Mkuu wa Majeshi Jenerali Mabeyo na makamanda wote kwa kazi nzuri ya ulinzi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kurudisha kambi ya JKT ya Mpwapwa. Hata hivyo kambi hiyo ina mapungufu yafuatayo:-

Kwanza ni kuhusu upungufu wa majengo, hivyo nashauri Serikali iwajengee majengo ya kutosha kwa ajili ya makazi yao na ofisi za kufanyia kazi. Pili, vitendea kazi kama vile magari, matrekta kwa ajili ya kilimo kwa kuwa eneo hilo ni zuri kwa kilimo na chakula kinachopatikana watumie wenyewe ili kupunguza gharama ya Serikali kupeleka chakula kambini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, JKT Mpwapwa ianze kuchukua vijana wa kujitolea wa form four na form six kama makambi mengine ya JKT. Katika JKT Makutupora majengo yafanyiwe ukarabati, vyombo vya usafiri viongozwe kama vile magari na kadhalika. Posho za askari Wanajeshi wa JKT na JWTZ ziongezwe. Majeshi yote yajengewe makazi badala ya kupanga uraiani, kambi zijengwe za kutosha ili wanajeshi wote wasipange mitaani. Usafiri katika majeshi yote hautoshi hivyo nashauri magari yaongezwe katika kambi zote ikiwemo Kambi ya Ihumwa, Makutupora na Mpwapwa. Posho ya chakula ya wanajeshi wote iongezwe haitoshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia huduma ya maji iboreshwe na barabara zikarabatiwe katika Kambi ya JKT Mpwapwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.