Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tabora una Kambi ya muda mrefu ambayo inaitwa Milambo Barracks. Kumekuwa na changamoto za uchakavu wa miundombinu ya barabara zinazozunguka kambi hiyo ya muda mrefu. Niombe Serikali iangalie mambo yafuatayo:-

Kwanza, ukarabati wa barabara, pili, ukarabati wa nyumba zao na tatu, ukarabati wa jengo la geti lililoko kabla ya kuingia ndani ya kambi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha niiombe Serikali kupeleka vifaa vya kisasa kwa ajili ya Hospitali ya Jeshi, ipeleke Madaktari Bingwa hususani wa magonjwa ya wanawake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuomba msaada huo kunatokana na kutokuwa na Hospitali ya Manispaa ya Wilaya na hivyo kusababisha watu wengi kwenda Jeshini kupata huduma hiyo. Miundombinu ya maji ikarabatiwe kwani ni michakavu sana.

Vilevile Serikali ilipe madeni ya maji/TANESCO ili kusitokee ukataji wa huduma hizo kwenye majeshi kwani kukatiwa huduma hizo ni aibu kubwa. Fedha za matumizi hayo zipelekwe kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali kupeleka fedha zilizoombwa bila kupunguza, pia kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba hii.