Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni Wizara muhimu kwa uhai na mustakbali wa nchi yoyote, bado naafiki Jeshi halisi la JKT kimuundo. Ningependa Jeshi letu liende katika usawa kivifaa, lakini imeonekana Jeshi kwa sasa halina powerful public branding ili kusimama kama taasisi yenye chapa ya Kitaifa. Wananchi hupata public relations ya Jeshi only wakati wa sherehe tu, na si vinginevyo na hivyo Jeshi hubakia katika obscurity. Bila shaka mazoezi ya kijeshi ni moja ya njia hizo kama ile amphibious iliyofanywa Bagamoyo. Ningependa Jeshi liji-brand pia kwenye kufanya kazi za dhamana mara zinapotokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa kuna dharura za mvua/upepo lakini Jeshi halijitokezi kikamilifu. Kazi hizo hufanywa kwenye matukio ya big magnitude tu. JKT inapaswa ipitie upya jukumu lile la kujenga uzalendo ambalo linaonekana limeshindwa hata katika hili, inafaa JKT ijitathmini upya.