Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Jeshi letu kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba hii naomba nichangie kwa kumuomba Mheshimiwa Waziri maana anajua na kama amesahau nimkumbushe, ni ukweli usiofichika Wilaya ya Kilindi katika Mkoa wa Tanga ni eneo ambalo linanyemelewa na watu wabaya wenye kuhatarisha usalama wa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo wananchi takribani 50 au pungufu wamekamatwa kwa kujihusisha na vikundi vya ugaidi na kwa kuzingatia jiografia ya Wilaya ile yenye misitu, milima mingi, hivyo kuwa ni sehemu ya kujificha. Nimuombe Mheshimiwa Waziri kwa kushirikiana na viongozi wetu wa Jeshi la Ulinzi kama taratibu zitaruhusu basi tupatiwe Kituo cha Jeshi ambacho kitasaidia kulinda amani ya eneo hili pamoja na Taifa kwa ujumla, tusisubiri mpaka hali mbaya ikatokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeyasema haya nikifahamu kabisa katika Mkoa wa Tanga tuna Kambi ya JKT iliyopo Wilaya ya Handeni lakini pana umbali baina ya Wilaya hizi mbili. Mimi naamini kabisa kuna gharama ya kuanzisha vituo hivi lakini usalama wa eneo hili ndiyo wa muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.