Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia kuhusu JWTZ wanaolinda mpaka - Wilaya ya Kakonko. Wapo wanajeshi wanaolinda mipaka ya nchi yetu kufuatia ujio wa wakimbizi Wilayani Kakonko. Wanajeshi hawa husumbua raia wanaotoka Burundi kuja kwenye masoko ya ujirani mwema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nimepata taarifa juu ya JWTZ kupiga Warundi waliokuja soko la Kabare, Kata ya Gwarama. Nashauri askari hawa watekeleze majukumu yao bila kuvunja sheria za nchi, wawe karibu na wananchi ili kujenga mahusiano mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ma-DC na RC kuvaa sare za jeshi; Wakuu wa Wilaya na Mikoa ambao ni wanajeshi wamekuwa wakivaa mavazi ya kijeshi wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao ya Kiserikali ofisini. Jambo hili huwapa hofu sana wananchi ambao hawajazoea kuona Mkuu wa Wilaya/Mkoa akawa ndani ya vazi la kijeshi na hivyo kushindwa kupeleka shida zao kwa wakuu hao. Huu si utawala bora pale ambao mtawala anaogopwa na wale anaowaongoza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mchakato wa vijana kujiunga na JKT; zoezi la kusajili vijana wanaojiunga na mafunzo ya JKT linagubikwa na vitendo vya rushwa sana na hivyo zoezi zima kutokuwa huru kwa raia wote.

Mheshimiwa Mwenyeikiti, Kambi ya JKT Kamembwa bado mipaka yake haijakaa vizuri kwani raia wa Kazilamihunda wanadai eneo lao linavamiwa na jeshi na hivyo kuleta malalamiko mengi. Nashauri ufanyike upimaji rasmi wa kuweka mipaka ukishirikisha viongozi wa Kijiji cha Kazilamihunda na uongozi wa Jeshi (Kambi ya Kanembwa).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa SUMA JKT ambapo ni jeshi la uzalishaji mali lielekeze miradi yake kufanyika/kupatikana kila kambi ili JKT zote nchini ziweze kutekeleza majukumu ya mradi huo bila kutegemea toka Dar es Salaam.