Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kutoa mchango wangu mdogo kwa ajili ya bajeti hii ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwa dhati ya moyo wangu nianze kwa kuipongeza Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama hasa Jeshi la Wananchi wa Tanzania na waswahili wanasema ukiona vinaelea ujue vimeundwa, nidhamu kubwa inayooneshwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania ni kielelezo cha utekelezaji bora wa sera za Chama cha Mapinduzi katika kipindi chote toka Taifa limepata uhuru. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, si siri, Jeshi la Wananchi wa Tanzania ni miongoni mwa majeshi duniani yenye nidhamu ya hali ya juu. Taifa letu la Tanzania tumepata sifa kitaifa na kimataifa, tumeshiriki operesheni mbalimbali duniani na Jeshi letu; ninataka nijivunie hata makamanda mliopo humu kwenye ukumbi; tunasema ya kwamba Chama cha Mapinduzi kinatakiwa kipongezwe kwa kuwa katika kipindi cha takribani miaka 50 ya Uhuru Jeshi letu limekuwa na nidhamu na dunia yote imetutambua kwa kazi kubwa inayofanywa na wapiganaji wetu.

T A A R I F A . . .

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli wa Chama cha Mapinduzi chini ya nidhamu ya Jeshi la Wananchi Tanzania huwezi ku-exclude kwa sababu utendaji na utekelezaji wa sera zote toka tumepata uhuru nchi hii imekuwa ikitawaliwa na Chama cha Mapinduzi, unawezaje ukakitenga Chama cha Mapinduzi, unawezaje ukaitenga CCM na mafanikio makubwa yanayopatikana kutokana na nidhamu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoja niwaambie Waheshimiwa Wabunge, nidhamu ya Jeshi letu na ndiyo maana hata leo mchana wakati kuna hoja zimetolewa juu ya vijana wa Jeshi la Polisi wamepigapiga risasi pale juu kidogo jana kwa sababu ya tukio lilikuwa limetokea kwa Mheshimiwa Malima. (Makofi)



Mheshimiwa Mwenyekiti, let me tell you one thing, tunapozungumzia nidhamu ya vyombo vya dola, unajua kuna mataifa mimi nimejaribu kutembeatembea kidogo duniani, kuna mahali haya mambo tunayoyaona Tanzania sisi tunayapuuza lakini nataka niwaambieni hawa wapiganaji wa Tanzania kama ni Bunge tukiamua leo tukasema kwamba kwa nidhamu wanayoionesha mimi natoa rai kabisa Waheshimiwa Wabunge kwa bajeti zinazokuja naomba Jeshi la Wananchi wa Tanzania tulipe kipaumbele cha kwanza kwa sababu wapiganaji hawa wameonesha nidhamu ya hali ya juu na Taifa letu limepata sifa kitaifa na kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende katika sekta nzima ya suala la JKT.

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa
Mwenyekiti, taarifa.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hizo interruption uzipuuze ili niweze kuendelea na mchango wangu kwa sababu nina muda mfupi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, JKT kama moja ya sehemu ya kuzalisha ajira, ninaomba nitoe ushauri kwa Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi. JKT, ninatoa ushauri, kwa sababu JKT ina-recruit vijana wengi wanakwenda kupata mafunzo, naiomba Serikali tutenge fedha za kutosha, vijana wanapokwenda JKT wakafanya training ya kijeshi, wakamaliza kwa kipindi cha miezi sita wapelekwe na watafutiwe mashamba makubwa wafanye uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii italisaidia Taifa kupata chakula lakini pia vijana hawa kwa kipindi hicho watakuwa wanapata ajira in phase, wamemaliza walichozalisha kinakuwa mali yao wanaondoka wanaingia wengine, hivi ndivyo wanavyofanya mataifa makubwa kama China na mataifa mengine duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ninatoa ushauri, wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania sasa hivi kuna chama chao kinaitwa MUWAWATA, huu ni umoja wa wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, kwa maslahi ya usalama wa nchi si sahihi sana umoja huu kuwa nje ya mfumo wa usimamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Hatari hii inaweza ikajitokeza wakaingiliwa na kuanza kulishwa sumu na kusababisha uasi kwenye nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, MUWAWATA waendelee kuwa na uratibu chini ya Serikali kupitia Jeshi la Wananchi kwa sababu hawa ni wapiganaji wa akiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina takwimu, miaka michache ya nyuma MUWAWATA ulikopeshwa bajaji na wakalipishwa hela nyingi na vikundi vya wafanyabiashara, this is very dangerous kwa security ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa ushauri, kaka yangu Kamanda Mabeyo najua uko hapa, kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwinyi, najua uko hapa kipenzi cha Watanzania, ninaomba upeleke hii proposal mkahakikishe kwamba MUWAWATA inakuwa chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.