Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MWATUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuwa na hali ya uzima na afya. Nishukuru ukumbi huu leo wote tuliopo hapa pia tupo wazima wa afya mpaka hivi sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi naomba kuchangia Hotuba hii ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nachangia kuhusu JKT hasa kwa vijana na kule kwetu Zanzibar. Kule Zanzibar kuna vijana wetu ambao wanakwenda JKT na wanakuwa wazuri tu wakirudi kule wameiva, lakini wakifika kule wanakuwa hawana ajira rasmi za kujiajiri, wanahangaika isipokuwa ajira zao ziwe mikononi mwao. Vijana hawa wanakuwa wanatupigia kelele sana sisi wazazi au kama hivi sasa mimi ni Mheshimiwa, lakini huko nyuma nakumbuka sisi Wabunge waliopita walikuwa wanapata hizi ajira kama kwa mtoto wake au mtoto wa ndugu yake lakini ajira walikuwa wanapata kwa mtu mmoja mmoja, kwa hiyo zoezi hili limeondoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi naomba hili zoezi lirudi tena sisi Wabunge tuwe mfano wa kupata kwa kila mtoto kama mmoja mmoja au katika jamii tulizonazo wapate ajira hizi za Jeshi ili na wao wajiajiri na wajisikie. Na wanakuwa na hamu sana ya kwenda Jeshini, lakini ajira kama tunavyozungumza ni ngumu. Hili lirudi na lizingatiwe sana ili wale vijana wawe na imani na Nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niwapongeze Jeshi kwa kazi zao wanazozifanya na hasa jana tu, wakati mimi nakuja huku Bungeni nipo maeneo ya Mlandizi, ilitokea ajali mbaya kati ya basi la Tanga na coaster inayotokea Morogoro, walisaidia roho za binadamu pale… (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MWATUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hiyo siikubali kwa sababu mimi sikusema kwamba huyo Mbunge ndiye anayetoa hiyo ajira hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nieleweke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umesikia, mimi naomba kwamba sisi Wabunge hivi sasa tunaomba kwamba zikitokea hizi ajira za Jeshi basi kama kuna uwezekano tuzipate ili tuwasaidie wale vijana na wale watoto wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea na hotuba yangu hii…majimboni, hata ikiwa majimboni ikiwa kwa jamii lakini tunaomba kwamba tupatiwe na sisi hizi ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi jana limeokoa roho za binadamu pale Mlandizi kati ya basi la Tanga na basi la coaster linalotokea Morogoro, ana-overtake basi la Tanga kwa bahati yule amejitahidi kulivusha lakini hakufanikiwa likaenda uso kwa uso dereva katoka miguu hana. Kwa hiyo, pale watu walishindwa kumtoa kila mmoja na imani yake basi walitokea vijana wetu hawa wa Jeshi na wakaenda pale wakaokoa roho zile wakawakwamua na palepale ikatokea gari wakapelekwa hospitali. Mimi ninawashukuru sana na ninawapongeza sana kwa kitendo kile walichokifanya jana.