Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili nichangie bajeti hii ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa niaba ya wananchi wangu wa Mtama nitoe pole kwa wenzetu wa Arusha kwa msiba mkubwa walioupata kutokana na ajali na kufiwa na wanafunzi karibu 32, tunaamini Serikali itachukua hatua kuzuia hizi ajali ambazo zimeendelea kutokea siku hadi siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani ilianza kuchukua hatua kadhaa za kuongeza mapato ya Serikali ikiwa ni pamoja na kubana mianya ya wakwepa kodi. Pia kupunguza matumizi ikiwepo kupunguza safari, kupunguza sherehe na matumizi ambayo kwa kweli pengine kwa namna moja au nyingine hayakuwa ya lazima; ikiwemo kushughulika na wafanyakazi hewa na hatua mbalimbali ambazo zilichukuliwa na Serikali katika kipindi ambacho Serikali imekuwepo madarakani. Pia kwa takwimu tunaambiwa uchumi unakua kwa asilimia 7.2. Haya yote hayatakuwa na maana kama hayatatafsiriwa kwenye maboresho kwenye huduma za jamii na hasa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua hizi lengo lake lilikuwa ni kuongeza uwezo wa Serikali. Sasa kama hatua hizi zimechukuliwa na matokeo yake ni chanya tunapaswa tuyaone kwenye ongezeko la huduma za jamii, na hapa tuanze na suala la maji ambalo linagusa kila mtu. Tusipofanya
hivi hatua tulizochukua hazitakuwa na maana hata kidogo.
(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti iliyopita tumetenga bilioni mia tisa. Bajeti hii tukiwa tumesimamia hatua tulizozichukua ambazo kwa kweli zingeongeza uwezo wa Serikali; tunatoka 900 kwenda 600, hatujatafsiri mafanikio ya hatua tulizozichukua, kwa vyovyote vile Watanzania hawawezi wakatuelewa. Ukuaji wa uchumi wetu hauwezi ukabaki kwenye makaratasi peke yake, hatuna tunayemfurahisha, tunataka tuwafurahishe wananchi wetu na hivyo, lazima tutafsiri ukuaji huu kwenye huduma za jamii na hapa kwenye sekta ya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wito wangu wa kwanza, naamini Serikali ni sikivu. Watu wamepiga kelele juu ya jambo hili lakini lazima pia tuone matokeo yake, wananchi hawataelewa hatua tunazozichukua kama haziwezi kwenda kubadilisha maisha yao ya kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ambayo bahati nzuri kwa mujibu wa Katiba ya CCM ilani hii inatengenezwa na kusimamiwa na Idara ya Itikadi na Uenezi, ambapo wakati ikitengenezwa mimi nilikuwa mkuu wa idara hiyo.

Vile vile nilibahatika kuzunguka nchi nzima, jimbo kwa jimbo na kwa kila jimbo nimelala siku moja. Tatizo la maji liko kila jimbo katika nchi hii, hakuna mahali ambako hakuna tatizo hili. Tunapishana ukubwa wa tatizo lakini umegusa kila mahali na mimi nimeshuhudia kwa macho yangu. Ndiyo maana tulipokuwa tunatengeneza ilani ya uchaguzi moja ya jambo kubwa ambalo tumelizungumza kwa kina ni suala la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ilani hii ya Uchaguzi, iliyotengenezwa na Chama cha Mapinduzi ndio mkataba wetu kati ya CCM na wananchi. Tusipoitekeleza wananchi hawataturudisha na huu ndio ukweli, kwa sababu tuliwaahidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya tatizo la maji pamoja na kuathiri watu wote lakini akinamama ambao ndio wapiga kura wakubwa wa CCM ndio waathirika wakubwa wa tatizo hili. Ndiyo maana sina mashaka kwamba Serikali itasikiliza iende ikaongeze pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye ilani hii tumeahidi kwamba tutatoa kiwango cha upatikanaji wa maji vijini kutoka asilimia 67 kwenda 85. Dar es Salaam pale ambapo DAWASCO na Luhemeja wanajitahidi kufanya vizuri lakini kama hakuna hela mambo yatakwama; tunataka kutoa 68 kwenda 95. Kwenye miji na makao makuu ya mikoa kutoka 86 kwenda 95, miji midogomidogo kutoka 57 kwenda 90. Hili halitafanikiwa tukienda na bajeti hii. Ndiyo maana naunga mkono hoja Serikali wasione aibu wala wasijisikie vibaya kurudi kwenda kuongeza pesa hapa. (Makofi)

Mwishoni nitatoa mapendekezo. Eneo la pili ni kwenye umwagiliaji. Umwagiliaji ukiangalia hapa hela iliyotengwa ilikuwa kidogo, hela iliyopelekwa asilimia 8.4 lakini hela yenyewe sijui kama wanajua kwamba sehemu kubwa imekwenda kuliwa. Tunayo miradi ya umwagiliaji; jimboni kwangu nina miradi mitatu ya umwagiliaji mradi mmoja umetumia miaka nane haujakwisha, mingine ipo kisingizio kikubwa ni kwamba ilibuniwa vibaya .

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya sana pale jimboni kwangu wakamfukuza Mkurugenzi ambaye hakuwepo, ambaye siye aliyebuni, waliobuni miradi na pesa zikazama wapo na wanaendelea kula nchi hawaguswi kwa lolote. Leo mafuriko tunayoyaona ni kwa sababu tumeshindwa ku-manage maji yanayotokana na mvua ambayo yanatiririka kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama tunaendelea kuona umwagiliaji kama kasehemu kadogo sana kwenye Wizara, nadhani pengine either it is wrong placed, tuipeleke mahali sahihi ili umwagiliaji ufanye kazi iliyokusudiwa, tukienda hivi hili eneo hatutafika. Sasa napenda nitoe mapendekezo yafuatayo:-

La kwanza, hiliā€¦

NAIBU SPIKA: Muda wako umekwisha Mheshimiwa.