Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

uchumi wa Taifa, pia imepita kwenye maeneo ya Viwanda vya Chai, Karatasi, Mgololo na Mbao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme; naomba Serikali ipeleke umeme Kata ya Mtambula, Idunda, Itandula, Kiyowela, Idete, Makungu na katika maeneo ya vituo vya afya na maeneo ya shule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maji; naomba kutengenezewa miundombinu ya maji. Kuna matanki ya maji 12 hayafanyi kazi sababu miundombinu ya maji imeharibika, ilijengwa 1970, naomba Serikali iitengeneze miundombinu hii ili kuondoa adha kwa wananchi wa Kata ya Igowole, Nyololo, Idunda, Itanduka na Kibao ambao wanapata shida kubwa ya kukosa maji safi na salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vituo vya Afya; naomba Serikali imalizie kujenga vituo vya afya katika Kata ya Mtwango, Mninga na Makungu. Wananchi wamejenga kuta bado kumalizia tu.
WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Naomba Mheshimiwa Mbowe…
MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa!..
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbunge naomba ukae chini. Jamani Waheshimiwa Wabunge, wakati wa wind-up hakuna taarifa. Naomba tuendelee na Waheshimiwa Mawaziri. (Makofi)
WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Jambo la kwanza niweke bayana kwamba wale wanaochangia, wasome kwanza mafungu maana yake nini. Mheshimiwa Mbowe alichanganya kati ya Fungu 62 na Fungu Na. 98. Fungu 62 ni Uchukuzi ambalo ni fedha za ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Bunge hili liliidhinisha shilingi bilioni 143.5 na hadi tarehe 31Machi, fedha ambazo zilikuwa zimetolewa ni shilingi bilioni 56.69. Fungu Na. 98 ni Ujenzi. Fedha za ndani ambazo Bunge hili liliidhinisha ni shilingi bilioni 798.26 na kati ya hizo, shilingi bilioni 606.64 zilikuwa ni kwa ajili ya Mfuko wa Barabara. Shilingi bilioni 191.62 ni kwa ajili ya miradi ya ujenzi, miradi mbalimbali, vivuko, madaraja na nyumba za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hadi kufikia tarehe 31 mwezi Machi, fedha zilizotolewa kwa ajili ya miradi, zilikuwa shilingi bilioni 931.3. Kati ya hizo, shilingi bilioni 323.95 zilikuwa ni za Mfuko wa Barabara. Shilingi bilioni 607.35 zilikuwa ndiyo za ujenzi wa nyumba, vivuko na kulipia madeni ya Wakandarasi. Sasa ukichukua fedha zilizoidhinishwa ukatoa zile ambazo zimekwisha tolewa mpaka sasa, zilizozidi ni shilingi bilioni 133.04 ambazo ni sawa na 0.6% ya bajeti yote ya mwaka ambayo ni shilingi trilioni 22.5.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inasema hivi, kwanza kwenye kanuni za sheria za bajeti kanuni ya 28(1) inasema, nanukuu: “All reallocations between Votes shall require the approval of the Minister.” Kwa hiyo, sheria imenipa mamlaka.
La pili, 28(2) inasema hivi, “reallocations between Votes shall not exceed 5% of the total Government Budget.”
Nimeshawapigieni hesabu hapa, zilizozidi ni 0.6%. Hakuna mahali popote ambapo sheria ya nchi au sheria ya bajeti imevunjwa. Ndiyo maana nasema huo ni uongo ulio dhahiri na kwa kiongozi kama yeye kutoa takwimu ambazo hazina ukweli ni upotoshaji wa Bunge, ni upotoshaji wa wananchi wa Tanzania. Serikali ya Awamu ya Tano ni makini, inasoma kwa kuzingatia matakwa ya sheria ya nchi na sheria zote zinazoongoza utekelezaji wa bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisemee hoja nyingine moja ambayo ilitolewa, ambapo ilishauriwa kwamba fedha zote za Mifuko ambayo iliundwa na Sheria za Bunge zipelekwe kama zilivyopitishwa na Bunge na ziende kwa wakati. Tunakubaliana kabisa na hiyo hoja na Serikali imeanza kuchukua hatua. Tumefungua account maalum kwa kila Mfuko ambao umeanzishwa ili kuhakikisha kwamba fedha hizi za Mifuko hiyo zinalindwa. Kwa hiyo, tahadhari tu hapa ni kwamba utoaji wa fedha hizi utategemea hali ya mapato katika kipindi husika, lakini Serikali imechukua hatua hii, tunaupokea ushauri, tutaendelea kuzingatia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kulisemea ni ushauri ambao tulipokea kwamba tozo kwenye mafuta ziwekwe kwenye Mfuko wa Maji na iongezwe kutoka Sh. 50/= hadi Sh. 100/= kwa lita ili kuondoa tatizo la maji. Hii ni hoja ya msingi na kwa upande wa Serikali tunasema, kwa sasa hivi, tunafanya uchambuzi wa mapendekezo ya wadau mbalimbali ili tuweze kurekebisha Sheria za Kodi na tozo ikiwa ni pamoja na haya mapendekezo ambayo Waheshimiwa waliyatoa. Kwa hiyo, napenda kuwahakikishia tu kwamba tutakapokuja mwezi wa Sita kuleta bajeti, ushauri mbalimbali ambao tumepokea, unafanyiwa uchambuzi na mapendekezo yanayotakiwa tutayaleta mbele ya Bunge lako Tukufu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika, kulikuwa na hoja inafanana na hiyo ambayo ilielekezwa. Kulikuwa na hoja ya Mheshimiwa Jitu ambayo alishauri kama hivyo kwamba tuweke tozo kwenye mafuta na fedha hizo tupeleke kwenye Mfuko wa Mazingira.
Ushauri kama nilivyosema, umepokelewa. Mheshimiwa Jitu Soni ndiye alitoa ushauri huu. Kama nilivyosema, tumeshafungua Akaunti Maalum na tutahakikisha kwamba hizo fedha tunazi-ring fence, lakini ushauri tumeupokea, tunaendelea kuufanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisemee hoja ya mwisho. Tulipokea ushauri kwamba ukuaji wa uchumi unatakiwa uende sambamba na kuongezeka kwa huduma za maji, umeme na miundombinu. Utekelezaji wa mipango na sera mbalimbali za Serikali, lengo lake ni kuhakikisha kwanza uchumi wa nchi unakua. Kama keki haikui, maana yake hicho tunachogawana ni kidogo mno. Kwa hiyo, ushauri wake ni mzuri kabisa kwamba tukuze kwanza ile keki na hapo ndiyo itatuwezesha kugawana vizuri na kupeleka huduma bora zaidi za jamii za umeme maji na miundombinu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na hoja na ushauri mzuri kwamba Serikali iangalie namna ya kuongeza bajeti ya Mfuko wa Pembejeo ili kuboresha Sekta ya Kilimo. Serikali inapokea ushauri huo na tunaendelea kuufanyia kazi kwa sababu nchi hii bila kilimo, nchi ya viwanda haitawezekana. Kwa hiyo, ni hoja ya msingi, tunaipokea na tutaifanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango huo, naomba kwa mara nyingine tena kuunga mkono hoja iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa asilimia mia mbili. Ahsante.