Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

NAIBU WAZIRI WA NIASHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa hii. Nianze na mimi kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi kubwa waliyofanya, pamoja na Katibu Mkuu. Hata hivyo, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa namna anavyosimamia rasilimali za nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yako mambo ambayo yamezungumzwa kwa wingi sana katika bajeti hii na yanahusu sana kwa kiasi kikubwa Wizara ya Nishati na Madini. Hata hivyo nitajielekeza sana kwenye hoja za nishati kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Spika, suala la LNG, suala la kiwanda cha kusindika gesi; Waheshimiwa Wabunge wameuliza kama mradi upo ama haupo.

Mheshimiwa Spika, nataka nilieleze Bunge lako Tukufu kwamba mradi wa LNG wa Lindi bado upo na wala hautahamishwa, hauendi Msumbiji wala sehemu yoyote. Na hapo tulipofika sasa tuko katika utekelezaji na tarehe 24 mwezi huu watalaam wanaondoka kwenda Trinidad & Tobago kwa ajili ya kukamilisha mazungumzo na wajenzi; na wajenzi watakaojenga ni makampuni makubwa ya ExxonMobil, BG Shell, pamoja na TPDC. Kwa hiyo, mradi huo upo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lipo suala la ujnzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda hadi Tanga.

Mheshimiwa Spika, nilitaka tu kutoa taarifa kwa sababu ni suala la maendeleo, tunajenga viwanda. Utaratibu wa ujenzi wa bomba hili umeshaanza na sasa nitoe taarifa sahihi kwamba bomba hili litafika katika mikoa minane ya nchi yetu na wilaya 24 na urefu wa kilometa 1,445 kwa kiasi kikubwa katika Tanzania. Hatua inayofuata katikati ya mwezi unaokuja tutasaini, lakini pia tutafanya uzinduzi na ujenzi wa jiwe la msingi huko Tanga katika eneo linaloitwa Chongoleani, Mjini Tanga. Kwa hiyo, ujenzi unaanza na utekelezaji utakamilika mwaka 2025. Kwa hiyo, Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta unaendelea vizuri.

Mheshimiwa Spika, mradi wa Makambako Songea; huu ni mradi muhimu sana. Wananchi walio wengi wa maeneo ya Mikoa ya Njombe, Songea na Wilaya zake wanautarajia sana mradi huu, uko katika hatua nzuri. Hata hivyo niseme tu commitment ya Serikali, kwa mwaka huu wa fedha tumetenga bilioni kumi na moja kwa ajili ya kwenye mradi huu, na ujenzi umeshaanza kufika katika hatua nzuri na mwezi Oktoba mwakani utakamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini niwaambie tu shughuli kubwa zinazofanyika katika mradi huu, ya kwanza kabisa ni ujenzi wa vituo vya kupoza umeme vilivyoko Madaba, Njombe pamoja na Songea Mjini na utakamilika hivi karibuni. Mradi mzima utagharimu Swedish Krona milioni 620, Dola za Marekani milioni 20 na shilingi bilioni 17 za Tanzania. Kwa hiyo, utekelezaji ukwenda vizuri mwezi Agosti mwakani utakamilika.

Mheshimiwa Spika, katika mradi huu kazi zitakazofanyika ni pamoja na kujenga transmission line ya urefu wa kilometa 250 kutoka Njombe hadi Songea, transmission ya kusambaza umeme katika vijiji 120 katika Wilaya nilizozitaja na kuwaunganishia umeme wateja 22,700. Kwa hiyo ni mradi mkubwa na unakwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kusambaza Umeme Mijini, maana wako Wabunge wamehoji kwamba tunapeleka umeme vijijini tu lakini mjini hatuendi. Niseme tu kwamba tumepata Dola za Kimarekani milioni 424 kwa ajili ya ujenzi na miundombinu ya mijini ili kuhakikisha kwamba
mijini tunakuwa na umeme wa kutosha ili viwanda vinavyojengwa mijini sasa viwe endelevu na kazi hii inafanyika vizuri. Kazi zitakazofanyika, ili nitumie nafasi hii vizuri, sana sana ni ufungaji wa transfoma kubwa na ndogo zinazoanzia KVA 50, KVA 100, KVA 200 hadi KVA 315. Hii ni katika kuhakikisha kwamba umeme mijini pia unaimarika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, REA Awamu ya Tatu; ninatambua kwamba muda ni mfupi sana, lakini niwape taarifa Waheshimiwa Wabunge kwamba tarehe 24 Juni (kesho kutwa tu) tunaanza sasa uzinduzi rasmi wa mradi mkubwa wa REA Awamu ya Tatu katika mikoa yote Tanzania Bara. Tunaanza na Mkoa wa Manyara tarehe 24, tarehe 4 hadi 5 tunakwenda Katavi na Rukwa, tukitoka Katavi na Rukwa tunaenda Mtwara na Lindi halafu tunaenda Kigoma. Kwa hiyo, wananchi wa Kagera Nkanda, Kazumulo pamoja na kule Kagera tutaendelea kuzindua hadi mikoa yote ikamilike kwa muda mfupi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, muda ni mfupi, lakini niendelee kuzungumza kidogo suala la usambazaji wa gesi majumbani.

Mheshimiwa Spika,…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzunguzaji)

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana kwa kunisikiliza.