Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya makadirio ya mapato ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Pamoja na kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri, naomba Jimbo la Mufindi Kusini tuliahidiwa kujengewa barabara kwa kiwango cha lami, barabara ya Nyololo hadi Mtwango, Mafinga hadi Mgololo, barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa, pia imepita kwenye maeneo ya Viwanda vya Chai, Karatasi, Mgololo na Mbao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme; naomba Serikali ipeleke umeme Kata ya Mtambula, Idunda, Itandula, Kiyowela, Idete, Makungu na katika maeneo ya vituo vya afya na maeneo ya shule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maji; naomba kutengenezewa miundombinu ya maji. Kuna matanki ya maji 12 hayafanyi kazi sababu miundombinu ya maji imeharibika, ilijengwa 1970, naomba Serikali iitengeneze miundombinu hii ili kuondoa adha kwa wananchi wa Kata ya Igowole, Nyololo, Idunda, Itanduka na Kibao ambao wanapata shida kubwa ya kukosa maji safi na salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vituo vya Afya; naomba Serikali imalizie kujenga vituo vya afya katika Kata ya Mtwango, Mninga na Makungu. Wananchi wamejenga kuta bado kumalizia tu.