Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niseme naunga mkono hoja hotuba hii ya bajeti ya Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapende kipekee kumpongeza sana Mheshimiwa dada yangu, Profesa Ndalichako pamoja na Mheshimiwa Injinia Manyanya, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na utendaji mzima wa Wizara hii kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wanaifanya katika usimamizi wa sekta yetu ya elimu, hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda tu kutoa ufafanuzi katika hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezitoa na tunashukuru sana kwa hoja hizo; la kwanza ni kuhusiana na ulipaji wa madai ya walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo madai ya malimbikizo ya mishahara vilevile yapo madeni ambayo yanahusiana na masuala mengine kama uhamisho, nauli na mengineyo ambayo siyo ya mishahara. Ukiangalia katika mwaka 2015/2016, tulilipa walimu 18,702 malimbikizo ya mishahara ya zaidi ya shilingi bilioni 13.9. Vilevile katika mwaka huu wa fedha katika kipindi cha Julai mpaka sasa tulipofikia, tumeweza kulipa madai ya walimu 12,037 yenye jumla ya takribani shilingi bilioni 12.6, vilevile tunaendelea kuhakiki madai yao, pia tumeendelea kuhakiki madai ya malimbikizo ya mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pia tumeendelea kuhakiki madai ya malimbikizo ya walimu 8,155 yenye jumla ya shilingi bilioni 9.7.

Ninashukuru sana kwa Wizara ya Elimu kupitia mradi wa P for R wameweza kulipa zaidi ya shilingi bilioni 10.5 na Serikali tumeshalipa zaidi ya shilingi bilioni 42.3 kwa watumishi mbalimbali ambao wana madai yasiyokuwa ya mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malipo mengine ya malimbikizo tunaendelea kuyafanya wakati wowote uhakiki utakapokamilika basi yataweza kulipwa. Kulikuwa kuna hoja kwamba wako ambao walipandishwa cheo au vyeo lakini walikuwa hawajarekebishiwa mishahara yao na Waheshimiwa Wabunge waliochangia hoja hii walitaka kufahamu ni kwa nini suala hili limejitokeza. Kama Wabunge watakumbuka tulipotoa uamuzi wa kuahirisha ajira mpya tarehe 13 Juni, masuala yote haya ya kimaendeleo ya kiutumishi nayo pia yalisimama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwahakikishie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba tunapoingia katika mwaka ujao wa fedha, watumishi ambao walikuwa wanastahili kupata vyeo vyao wataweza kurekebishiwa na kupata vyeo sahihi vya kimuundo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge katika suala zima la upandishwaji wa vyeo, katika mwaka ujao wa fedha 2017/ 2018, tumetenga au tumekasimiwa kupandisha vyeo watumishi wa umma 193,166, kwa hiyo tunaamini tutakuwa tuko vizuri na wote wanaostahili kupata vyeo vyao kwa mujibu wa sifa zinazohitajika na vigezo basi wataweza kupandishwa vyeo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na hoja ya hospitali ya Mloganzila kwamba inashindwa kufaya kazi kutokana na upungufu wa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kusema kwamba tumeshapeleka watumishi 50 na katika ajira mpya ambazo tumetoa kibali cha Wizara ya Afya na TAMISEMI 258 tumewapelekea tena watumishi wengine kumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo walikuwa na nafasi wazi 213, kitu ambapo tunachokifanya sasa tumewapa kibali na kuwahamisha kutoka kwa watumishi wengine walioko ndani ya Serikali na tayari kati ya idadi hiyo 213, watumishi 109 wamesharipoti na tunasubiri hao 104 wengine tunaendelea kujaza nafasi zao kwa njia ya uhamisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea pia na tunatarajia kabla hatujamaliza mwaka huu wa fedha, tutatoa pia kibali cha ajira mpya kwa Mloganzila 105 mpaka tutakapomaliza mwaka huu wa fedha mwezi Juni, watakuwa wamepata watumishi wapya 378 na tutaendelea kufanya hivyo mwaka hadi mwaka kuhakikisha kwamba wanapata Ikama ambayo wanaweza wakafanya nayo kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa kuna hoja ya upungufu wa walimu pamoja na wataalam wa maabara. Tayari tulishatoa kibali na tumeanza na Walimu wa Sayansi 4,129 na tayari ofisi ya TAMISEMI imeshawapangia vituo wameshaanza kazi. Vilevile tumetoa kibali cha Wataalam wa Maabara 219 na tayari 137 hadi sasa wameshapatikana na tutaendelea kufanya hivyo.