Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja hii. Waziri na timu yake hongereni sana kwa kazi. Ninayo mambo machache ya kuishauri Serikali na Wizara hii.

(a) Wazo la eti wasichana wanaopata mimba, warejeshwe shuleni ni dhahiri halina mashiko na halina msingi. Hatuwezi kuanza karne hii eti kuhamasisha watoto wa kike akipata mimba arejeshwe shuleni. Hii haikubaliki, haifai na kama Bunge tusishabikie jambo ambalo madhara yake ni makubwa sana. Tuendelee kupiga vita tabia ya zinaa mashuleni.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, vitabu vya kufundishia visivyo na ubora ambavyo vimeshasambazwa mashuleni kwa mamilioni:-

(i) Vitabu hivyo vyenye makosa viondolewe mashuleni haraka iwezekanavyo.

(ii) Waliohusika na ujinga huo wawajibishwe ikiwa ni pamoja na kuwastaafisha kazi zao hata ikibidi kuwafukuza. Ni jambo la aibu sana kwa Serikali yetu na kwa Chama chetu cha Mapinduzi.

(iii) Fedha na gharama iliyotumika kuchapisha vitabu hivyo ilipwe na wahusika haraka sana ikiwa ni pamoja kuwafilisi mali wanazomiliki ambazo zitakuwa zimepatikana kwa wizi na udanganyifu huo.

(iv) Walioviandika vitabu hivyo na makampuni yao wasipewe kazi hiyo tena. Wasipewe tender tena za kuandika na kuchapisha vitabu.

(c) Chuo cha FDC Kasulu; chuo hiki ni kikongwe sana na kimechakaa, kilijengwa mwaka 1974. Ninaomba sana chuo hiki kiwemo katika vile vyuo kumi vitakavyofanyiwa ukarabati, kama hotuba ya Waziri ilivyobainisha ukurasa wa 93 – 94. Mkoa wa Kigoma upo nyuma sana kielimu na hata kiufundi. Kigoma na hususani Kasulu tuna kila sababu ya chuo chetu kuongezewa ubora wake wa miundombinu.

(d) Kuhusu maktaba ya Wilaya ya Kasulu; ninaomba sana Wizara ya Elimu iangalie uwezekano wa kukamilisha jengo lenye ghorofa moja la maktaba ya Wilaya ya Kasulu ambalo lilianza kujengwa 2007 kwa nguvu za Mbunge wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu. Jengo hilo linahitaji vifaa vifuatavyo:-

(i) Finishing ya Ndani (milango, ceilings, gates na kadhalika).

(ii) Kuboresha mazingira ya nje ikiwemo kujenga uzio wa tofali ili kuimarisha eneo hilo.

(iii) Gharama ya takribani shilingi milioni 200 - 300 inaweza kabisa kukamilisha jengo hilo na likaanza kutumika. Wizara isaidie nguvu na juhudi ambazo tayari Wilaya imefanya.

(e) Kusaidia kukamilisha maabara za sayansi zilizopo katika Mji wa Kasulu. Majengo ya maabara katika shule zetu nyingi za sekondari zipo katika hatua mbalimbali kuanzia asilimia 40 hadi 70 za ujenzi. Wizara kwa kutumia fursa mbalimbali kama vile P4R Programs na Equip Tanzania Projects inayotekelezwa katika Mkoa wa Kigoma. Ni vizuri juhudi za pamoja kati ya Wizara na Halmashauri zetu tuwe na mpango wa kukamilisha maabara hizi, ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hongera kwa kazi, naunga mkono hoja.