Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KEPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mtwara haujafanya vizuri mitihani ya darasa la saba hata kidato cha pili. Moja kati ya sababu zilizotufikisha hapo ni uhaba wa walimu, Mkoa una upungufu wa walimu kwa asilimia 40. Baadhi ya shule za msingi zina walimu watatu wakati madarasa ni saba.

Je, watafundishaje? Tunaomba Wizara inapoajiri walimu izingatie kuwa Mkoa wa Mtwara una upungufu mkubwa hivyo wapewe walimu wengi ili walingane na mikoa mingine.

Suala la pili ni vuguvugu la kufuta ujinga wa kutojua kusoma na kuandika limepungua sana. Waratibu wa Elimu Kata zamani walikuwa wasaidizi wa EWW. Idadi ya wananchi wasiojua kusoma na kuandika inaongezeka mwaka hadi mwaka, Wizara ifufue na iweke mkakati wa kufufua EWW. Waratibu wa Elimu Kata hawana kazi nyingi wapewe jukumu la kusimamia EWW kama ilivyokuwa hapo zamani.

Tatu, hali ya taaluma katika shule za msingi na sekondari hairidhishi na hii inasababishwa na shule zetu kutokaguliwa, wakaguzi hawatoshi na hawana usafiri. Serikali iongeze idadi ya wakaguzi na wapewe usafiri wa uhakika ili waweze kukagua shule zao zote. Naunga mkono suala la kuifanya Idara ya Ukaguzi kuwa Wakala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.