Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani iliyosomwa na Mheshimiwa Susan Lyimo, Waziri Kivuli wa Elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mazingira ya shule za kata kutokuwa na mabweni, pia umbali na kutokuwa na ulinzi wa wanafunzi hasa wa watoto wa kike huko vijijini tunakotoka, umaskini wa kipato wa wazazi hupelekea wazazi kuwapangia nyumba watoto karibu na shule au wanafunzi kusafiri umbali mrefu kwenda shuleni. Watoto wa kike hukumbana na vikwazo vingi kama ubakaji, ushawishi wa pesa za kujikimu kutokana na kuishiwa kabla mzazi hajampa matumizi, elimu ndogo ya uelewa na ukosefu wa walimu na kusababisha utoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo naishauri Serikali ifuatilie na iwapo mtoto wa kike (mwanafunzi) akapata mimba kwa sababu hizo au nyingine na kwa kuwa anatoka familia za maskini awekewe utaratibu wa kuendelea na masomo ili apambane na umaskini wa kipato. Pia naunga mkono mapendekezo ya Kamati ya Bunge kuhusu suala hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya madarasa, walimu, vyoo, maji shuleni ni tete sana kupelekea kuporomoka kwa elimu. Hivyo, bajeti hii iangalie na kutatua kero hizo. Wananchi wamechangia kwa kujenga maboma ili Serikali imalizie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la madeni ya walimu, kupanda madaraja walimu na posho ya mazingira magumu, navyo ni kero kubwa na kupelekea walimu kushusha morali ya kazi na kushuka kwa elimu hasa shule za vijijini kutokana na mazingira magumu. Serikali ione haja ya kuwezesha maslahi ya walimu ili kuinua elimu. Kitengo cha ukaguzi nacho kiwezeshwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kuwasilisha.