Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Nawapongeza Mawaziri na watendaji kwa juhudi wanazochukua, ushauri kwa Serikali itoe fedha kwa wakati na za kutosha ili kupunguzia Wizara hii shida inayoendelea sasa hivi inayopelekea elimu kushuka.

Ninashauri juu ya ndoa za utotoni na mimba za utotoni, ninaiomba Serikali itoe elimu ya kutosha ili watoto wajue mabadiliko ya maumbile yao. Hivyo basi, naishauri Serikali kuridhia sheria ya watoto wanaopata mimba warejeshwe shuleni kwa masharti ambayo hayatafanya wanafunzi hao kurudia kosa hilo.

Pia ninaishauri Serikai iendelee kuandaa mazingira rafiki kwa watoto wa kike kupata elimu bila vikwazo vya kumrudisha nyuma. NIishauri Serikali kuimarisha vyuo vya FDC nchini ambavyo vitasaidia kuelimisha vijana wetu na kujiajiri mfano, FDC Kibaha ina mapungufu mengi sana. Niishauri pia Serikali kukagua shule binafsi nyingine ni za ovyo hazina vigezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ijitahidi kulipa madai ya walimu ili kuwatia moyo, hivyo BRN kufikiwa kwani huwezi kupata matokeo makubwa bila kuwekeza kwa walimu. Mikopo ya elimu ya juu iangaliwe kwani hakuna haki na weledi kwa watoaji wanaotakiwa kupewa wanakosa na wasiostahili ndio wanapata, Serikali iangalie hilo.