Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya elimu ni bajeti finyu sana ambayo haiwezi kukidhi mahitaji ya elimu ya nchi hii. Angalau elimu ipangiwe asilimia tatu ya GDP kama nchi za wenzetu katika Afrika Mashariki ambapo huanzia asilimia nne hadi asilimia saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu re-entry policy; watoto wa kike wanaojifungua wakiwa shuleni wawekewe sera ya kurudi kuendelea na masomo baada ya kujifungua, sera hii itasaidia watoto hawa kupata haki ya elimu (right to education). Aidha, itapunguza idadi ya wasio na elimu nzuri nchini na pia kupunguza idadi ya wasio na ajira nchini. Nchi nyingi zimefanikiwa katika hili, mfano ni nchi ya Zambia. Wapo Wabunge waliofanya utafiti juu ya hili na wadau wa nchi hii waliafiki wanaobeba mimba warudi shuleni kuendelea na masomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ubora wa elimu nchini; elimu bora hutolewa na walimu bora ambao wanalipwa vizuri na Serikali, wana mahali bora pa kuishi, wana madarasa ya kutosha na hakuna mlundikano wa wanafunzi darasani. Aidha, walimu walipwe stahili zao mapema kuondoa malalamiko ili wafanyekazi wakiwa na amani moyoni.

Aidha, miundombinu ya elimu kama uhaba wa walimu mashuleni, uhaba wa madarasa na madawati, uhaba wa vyoo, uhaba wa maji safi na salama na uhaba wa vitabu, chaki na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu makato ya mishahara bila ridhaa, walimu wamekuwa wakikatwa mishahara yao bila ridhaa yao jambo ambalo ni kinyume cha Sheria za Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2013 makato hayo ni kama vile ya kwenye ujenzi mbalimbali wa majengo ya umma; kwa mfano, maabara, madarasa na kadhalika. Makato mengine ya NIC toka mishahara ya walimu wa Wilaya ya Kakonko wanaozidi 14 bila mikataba yoyote. Makato haya ni wizi wa mishahara ya walimu kwani hata kwenye salary slip makato hayo hayaonekani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kusimamisha kazi walimu kwa kigezo cha wanafunzi ku-fail. Hili halikubaliki kwani ni wahalalishaji tu. Aidha, wakuu hawa hufikia hatua ya kuwashusha vyeo Walimu Wakuu kwa kigezo cha wanafunzi ku-fail bila kujali miundombinu mashuleni.

Kuhusu kuundwa kwa TSC toka iliyokuwa TSD hakujaleta mabadiliko yaliyokusudiwa, mfano TSC ilitakiwa:-

(i) Iwe ndio mwajiri/afunge mikataba na walimu;
(ii) Ilipe mishahara;
(iii) Ipandishe madaraja;
(iv) Iadhibu walimu (nidhamu); na
(v) Itoe barua ya kustaafu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo yake mwalimu amendelea kuhudumiwa na Wizara, Idara nyingi sana hivyo kuleta ugumu kwa walimu katika kuhudumiwa.