Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia. Ni hotuba nzuri, inatoa dira wapi tunaelekea katika kuinua kiwango cha elimu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri, aiangalie sana Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe. Wilaya hii kitaalam ndiyo inayoongoza katika Mkoa huu na iko katika nafasi nzuri sana kitaifa kwa miaka mitatu. Nakuomba uidhinishe tuanze kidato cha tano na sita kwenye shule tatu za Makoga, Wanike na Wanging’ombe na nitakushukuru sana zingeanza mwaka huu. Tayari madarasa na mabweni kwenye shule za Makoga, Wanike na Wanging’ombe yamekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wilaya ya Wanging’ombe ijengewe Chuo cha VETA. Lipo eneo Soliwaya limeshaandaliwa kwa ajili ya kujenga Chuo cha VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishukuru sana Wizara kwa msaada wa kuboresha miundombinu ya shule ya sekondari ya Usuka na shule za msingi za Dalami na Ilembule. Naomba mpango huu uendelezwe mwaka huu katika shule ya sekondari ya Igosi na shule za msingi za Wanging’ombe, Palangawamu, Mtapa na Saja. Majengo hayo yamechoka sana kupita maelezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie tena kuwapongeza na kuwatakia kila heri.