Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hoja ya kuwarudisha watoto wajawazito waliojifugua shuleni; turejee mifumo ya elimu duniani yaani formal education na non-formal education. Fursa ya elimu kwa waliopata ujauzito ipo kupitia non-formal. Serikali iimarishe non formal system.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu lugha ya kufundishia; Sera ya Lugha ya Kufundishia inakinzana na ukuzaji wa fikra za kibunifu na kujiamini. Kiswahili kama lugha ya kwanza kwa walio wengi ndiyo lugha sahihi ya kufundishia. Kiingereza na lugha nyingine zibaki kuwa masomo tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuta ujinga au kuongeza idadi ya wanaojua kusoma na kuandika, Serikali izingatie umuhimu wa kuwa na Taifa lililoelimika kwa kuwatazama wasio na fursa ya kujiunga na formal education. Inakadiriwa watu milioni sita hawajui kusoma na kuandika. Hii ni hatari kwa ustawi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mabadiliko ya mitaala, kuna umuhimu wa kuimarisha dhana ya uzalendo ndani ya somo la uraia. Watoto au Watanzania wajifunze kuwa kuzaliwa Mtanzania ni jambo bora zaidi kuliko kuzaliwa mahali popote pale duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wajifunze falsafa hususan kipengele cha namna ya kufikiri (systemic and systematic thinking)logical reasoning na kadhalika.