Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Chuo cha VETA Ushetu, nchi yetu imekuja na dhamira ya kuifanya Tanzania iwe nchi ya uchumi wa kati na nchi ya viwanda. Hii itafanya wananchi kupunguza hali ya umaskini. Pia kufanikiwa ajenda hii, jitihada zifanyike ila siyo tu kutoa ajira hususan kwa vijana bali ni kuhakikisha nguvu kazi inatumika kwenye uzalishaji. Hivyo kunahitaji vijana wetu wawe na skills za kutosha kutoa mchango wao muhimu kwa ukuaji wa uchumi. Hivyo tunaomba Serikali yetu itujengee Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Ushetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ushetu inazo fursa za kutosha kufanya chuo hicho kilete tija kwa kuwa eneo hili ni kiungo kwa vile tunapakana na mikoa mitatu ya Geita, Kigoma, Tabora pamoja na Shinyanga yenyewe. Ni rahisi wananchi wa mikoa hii kufika Ushetu.

Pili, Ushetu kunapatikana rasilimali za kutosha za mazao ya misitu, mazao ya kilimo na kadhalika.

Tatu, Ushetu kunapatikana ardhi ya kutosha ambayo haina gharama. Wananchi wake wanao ushirikiano na wanajituma na wanapenda sana maendeleo.

Mhehimiwa Spika, namalizia kwa kusema tunomba sana Chuo cha VETA haraka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.