Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri, Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako, Naibu Waziri, Mheshimiwa Injinia Stella Manyanya na Katibu Mkuu wa Wizara kwa kazi nzuri na hotuba iliyosheheni utaalam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule kongwe zenye historia kubwa hapa nchini ni pamoja na Tabora Girls ambayo imetoa viongozi wengi lakini ina hali mbaya hasa kukosa uzio. Pamoja na hayo, watu wamevamia na kujenga kwenye eneo la shule. Hivyo, niiombe Serikali inapotoa fedha za ukarabati iangalie shule hiyo. Bwalo la chakula kwa wanafunzi hao ni la muda mrefu na miundombinu yake haifai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule kongwe nyingine ni Tabora Boys na Milambo. Shule hizi ni muhimu sana katika historia ya nchi hii. Ni shule zenye kumbukumbu na historia kubwa ya Baba wa Taifa, lakini hazina uzio, majengo ni machakavu sana pia hata miundombinu ya maji ni hatari kwa afya zao na matundu ya vyoo ni machakavu. Nashauri pamoja na uhaba wa fedha ni vema wakaanza ukarabati huo kwani wanafunzi wanateseka sana. Ningeomba sana mchango wangu uangalie kwa jicho la huruma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu madai ya walimu naomba yazingatiwe na yalipwe kwa wakati. Vilevile ukarabati wa shule ni vema uende sambamba na ukarabati wa nyumba za walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto ya wazabuni kutolipwa madai yao. Wazabuni hawa wanaolisha shule wanadai fedha nyingi na kusitisha huduma kimya kimya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.