Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu juu ya kukithiri wa masuala ya ngono katika vyuo vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyochangia kwenye mchango wangu wa maneno kuwa ni kweli tulipofika leo masuala ya ngono yameonekana yanahusika moja kwa moja katika kupandisha alama ya ufaulu na imefanya wanafunzi wenye uwezo mdogo kuonekana kuwa vinara kwenye ngazi ya ufaulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri kwa Serikali kutokana na mchango wangu juu ya ukithiri wa ngono vyuo vikuu. Ombi langu kwa Serikali ni kwamba kama ilivyofanya kwenye wasilisho la Miscellaneous Amendement na adhabu zake kwa yeyote atakayempa mimba mwanafunzi aliyekuwepo masomoni ama kumuoa mwanafunzi basi adhabu yake iwe ni miaka 30 jela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe kwa unyenyekevu mkubwa Wizara ya Elimu ituletee muswada wa sheria kwa walimu wote vyuo vikuu watakaobainika kuwa na mahusiano na wanafunzi basi adhabu ya kwanza iwe ni kusitisha ajira na kufungiwa miaka kadhaa bila kuajirika mahali kokote sambamba na adhabu ya kichapo cha hadharani ili kukomesha kabisa tatizo hili. Ni ushauri wangu adhabu pia itoe option ya kifungo jela.

Pamoja na adhabu niliyopendekeza pia ni rai yangu kwa Bunge lako Tukufu, Ofisi ya Spika iridhie ombi langu la uwepo wa special register book itakayobainisha usajili wa makosa ya ubakaji, ulawiti, ndoa za utotoni/wanafunzi na hata watuhumiwa wote vyuo vikuu waliobainika kuwa na mahusiano na wanafunzi vyuo vikuu ili iwe rahisi kwa sisi Wabunge kufanya follow up ya makaosa haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango juu ya uandaaji wa rasilimali watu kwa ajili ya usafiri wa anga ili kuweza kupata tija kamili kulingana na uamuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuoanisha na kuendeleza Shirika la ATCL; pamoja na mchango huu pia napenda nimshukuru sana Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako pamoja Mheshimiwa Mbarawa kwani baada ya juhudi zangu za kuonana na uongozi wa wanafunzi NIT sambamba na kikao cha tarehe 30/01/2017 na Mkurugenzi Mtendaji Shirika la ATCL nilibaini changamoto kubwa inayowakabili wanafunzi wa NIT hususani vijana wanaochukua mchepuo wa Aircraft Maintenance Engineering.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafunzi tajwa wana changamoto ya ada kubwa isiyohimilika kwa wazazi walio wengi ambao wengi wao wameonekana kuwa na uchumi mdogo usiohimili ukubwa na uzito wa ada iliyopendekezwa na NIT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi ya Rwanda katika ku- promote expertiseya masuala ya usafiri wa anga walianza kwa kuandaa rasilimali watu kutoka katika nchi yao. Ada kwa masomo ya Engineering ni kiasi cha shilingi 40,000,000 na masomo ya urubaini ada (direct fee) ni kiasi cha shilingi 80,000,000 na katika kukabiliwa na changamoto ya uandaaji wa rasilimali watu kwa ajili ya usafiri wa anga, nchi ya Rwanda iligharamia masomo ya wanafunzi wa fani ya usafiri wa anga kwa asilimia 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, kwa nini nchi yetu tunapata vigugumizi katika kukabiliana na kiasi cha ada ya shilingi milioni kumi kwa masomo yanayopatikana ndani ya nchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafunzi hawa wanahitajika kuanza practical training this June lakini hata ndege ya mafunzo hakuna. Katika mazungumzo yangu na Mheshimiwa Profesa Mbarawa hivi majuzi nilielezwa Chuo cha NIT pamoja na Shirika la ATCL wamejipanga kukodi ndege za mashirika binafsi ili wanafunzi waweze kufanya practical training.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tumenunua ndege mbili, focus yetu ni kuwa na ndege sita, sasa kwa nini mafunzo haya ya practical training NIT yasipewe kipaumbele? Kwani kufika kukodi ndege kwa ajili ya practical training na ilihali tunayo ndege ya Shirika la ATCL ipo Mwanza, ambayo inahitaji matengenezo kidogo na badala yake tukodi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoteza matumaini kwani wakati Mheshimiwa Rais anapambana ili kutujengea utamaduni wa kuondokana na matumizi yasiyo na umuhimu na kubana rasilimali fedha ya Taifa, lakini baadhi ya Taasisi bado tunaona Serikali ina fedha ya kupoteza kwa kufika kukodi ndege za mashirika binafsi kwa makusudi ya kufanikisha practical training (PT) yaani mafunzo kwa vitengo kwa wanafunzi wetu wa NIT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba huwezi kuandaa engineer wa masuala ya ndege bila kumpa mwanafunzi elimu ya vitendo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali ni kama ifuatavyo:-

(i) Ndege ya Shirika la ATCL iliyoegeshwa (park) Mwanza ipatiwe fedha na Wizara ya Fedha chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na chini ya usimamizi wa karibu wa Wizara ya Elimu ili kwa pamoja tumsaidie Mheshimiwa Rais katika kuimarisha usafiri wa anga ili kwa pamoja tuweze kuimarisha uchumi wa nchi yetu.

(ii) Ni ushauri wangu Serikali kupitia Wizara ya Elimu iweze ku-revive Civil Aviation Training Fund ili kwa pamoja tuweze kuifikisha elimu stahiki kwa walengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa furaha na imani kubwa naomba kuunga mkono hoja wasilisho la Bajeti Wizara ya Elimu kwa asilima mia moja.