Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja hotuba ya Kambi ya Upinzani na ile ya Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule zetu huko vijijini zina matatizo mengi. Hakuna mabweni kwa ajili ya wanafunzi wala walimu wa kutosha. Watoto wa kike wanapangiwa vyumba vya kulala kwa kukosa mabweni, huko wanarubuniwa na kushawishiwa kwa kuwa hukosa pia fedha za kujikimu kwani wazazi wakati mwingine hawawapi kutokana na umaskini walio nao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wa kike huweza kubakwa na kupata mimba, hivyo ninashauri Serikali ione namna ambavyo mtoto huyu anayepata mimba atakavyoweza kupata elimu baada ya kujifungua. Imekuwa kama adhabu kwa sababu tu ya kuwa ni wa jinsi ya kike kwani kama kijana aliyempa ujauzito huendelea na masomo hata kama sheria ipo hatujaona utekelezaji wake. Tunaomba Wizara ione hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la VETA tunaomba lipewe kipaumbele pamoja na FDCs ili wale watakaopewa kipaumbele kwa sehemu hizo wapate mafunzo na kuweza kujiajiri pindi watakapomaliza na hasa kupunguza wimbi la ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirejee katika Mkoa wa Iringa. Wazazi wameweza kujenga ama kuhamasisha ujenzi wa mabweni kwa ajili ya wasichana hasa shule ya sekondari Lyandembela Ifunda Mkoa wa Iringa na sekondari ya Mseke. Tunaomba Wizara iweze kushirikiana na TAMISEMI kuweza kusaidia katika umaliziaji wa majengo haya pamoja na kugaiwa walimu wa masomo ya sayansi, walimu watakaokuwa walezi wa wanafunzi kwa ajili ya kufundisha unasihi. Mheshimiwa Waziri utakapohitimisha uweze kutueleza mkakati wa kuwa na walimu wa ushauri nasihi mashuleni hasa shule za sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.