Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JAPMheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni hifadhi ya jamii. Kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi iliazimia kuanza kuwalipa pensheni wazee wote waliofikia umri mkubwa bila kujali walikuwa waajiriwa au laa, je, ni lini hasa ahadi hii ya kulipa pensheni kwa wazee hawa ambao wanaisubiri sana itatekelezwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, ni kwa lini Sera ya Hifadhi ya Jamii itaanza kutekelezwa kwa wananchi wote yaani wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara ili kila mwananchi afaidi mafao ya hifadhi ya jamii? Pia kuna mkakati gani wa kupunguza malalamiko ya wananchi ambao husumbuliwa sana na Mifuko ya Jamii kama NSSF na PPF? Je, hatua za kuboresha mifumo hii zimechukuliwa vipi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, sekta binafsi. Hivi sasa sekta binafsi ndiyo mhimili mkuu wa kukuza uchumi wa nchi yetu ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa wananchi wengi zaidi. Hata hivyo, waajiri wengi wa sekta hii hususani kilimo, ulinzi, huduma za hotelini, biashara na viwanda wamekuwa hawatoi mikataba na barua za ajira na wakati mwingine masharti ya kazi ni magumu sana na ya kinyonyaji, mazingira yanatisha sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia baadhi ya waajiri hulipa mishahara duni ambayo haiendani na uzalishaji na haina tija. Lazima Serikali ihakikishe kwamba waajiri wote wanakuwa na mikataba na barua za ajira zinatolewa kwa wafanyakazi wote. Hili liende sambamba na kuimarisha Idara ya Kaguzi za Kazi ili ifanye kazi ya ukaguzi mara kwa mara na kutangaza hadharani waajiri ambao wanakiuka sheria za kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Serikali kuboresha kilimo. Ni lazima Serikali ije na makakati mpya wa kuinua kilimo ikiwa ni pamoja na kuboresha mfumo wa ruzuku, usambazaji wa pembejeo, masoko, chakula, kama vile kahawa, mahindi, maharage na kadhalika. Je, Serikali imefanya uchambuzi ili kuimarisha kilimo kwenye maeneo yenye tija na kujenga mazingira wezeshi ili kuongeza thamani ya mazao? Nashauri pale ambapo wananchi wanaweza kuuza nje mazao yao waruhusiwe kwani itasaidia kuongeza fedha za kigeni. Pia mkakati wa kuanzisha kilimo kikubwa ili kutoa ajira kwa vijana wetu umefikia wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, ni mkakati wa kuanza kutengeneza magari na vipuli. Serikali lazima ifanye maamuzi magumu ya kimkakati ili kuanzisha kiwanda cha kutengeneza magari na vipuli vyake. Kiwanda hiki kitasaidia kuchukua vijana wetu wengi ambao wana ufundi mkubwa. Kuna mafundi wazuri katika mikoa yetu. Ni muhimu kuanza kutengeneza magari ambayo yatatumia gesi na mafuta. Pia itasaidia kufanya utafiti na kuziangalia projects za wanafunzi wa vyuo vya ufundi ambazo ni nzuri sana. Maamuzi haya ni muhimuHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kwenye maeneo yafuatayo:
sana ili kutoa ajira na kuokoa fedha za kigeni zinazotumika kununulia magari na vipuli.