Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru Mungu kwa kunipatia fursa hii ya kuweza kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya nchi yetu tuna changamoto kubwa ya mimba za utotoni zinazopelekea watoto wa kike kuacha shule. Suala hili ni vyema Serikali ikachukua hatua kwa kuhakikisha elimu ya afya ya uzazi inatolewa mashuleni ili watoto waweze kutambua mabadiliko ya miili yao na kuwawezesha watoto kufanya maamuzi sahihi. Serikali ihakikishe kuwa clubs za wasichana zinaundwa mashuleni na kila shule iwe na matron au mwalimu wa kike atakayewajibika kusimamia clubs hizo na utoaji wa elimu ya afya ya uzazi (sexual reproductive health).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la utoro mashuleni ambapo watoto wa kike wengi wanakuwa watoro kutokana na suala la menstruation period ambapo mtoto wa kike anaingia kwenye siku zake kwa siku tatu hadi nne ambapo kwa mwaka hufanya siku 48. Kama mtoto hatapata sanitary pads, atashindwa kwenda darasani na hivyo kuathiri ufaulu wake darasani au kupelekea watoto wa kike kuacha shule kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali itoe ruzuku ya sanitary pads kwa watoto wa shule ambapo watoto watapata sanitary pads (taulo za kujihifadhi) kwa bei rafiki ya shilingi 500 kwa pakiti badala ya shilingi 3000 hadi 4000 ya bei ya sanitary pads kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iongeze pesa za mkopo wa wasichana vyuoni ambapo waongezewe shilingi 40,000 kwa semister au shilingi 80,000. Ongezeko hili litasaidia wasichana kumudu mahitaji yao ya pads. Pendekezo la shilingi 40,000 na shilingi 80,000 linatokana na bei ya sanitary pads kwa sasa.