Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Lushoto ni Wilaya yenye wakazi zaidi ya 600,000 na Wilaya yenye majimbo matatu ya uchaguzi. Hata hivyo Wilaya ile haina Chuo cha VETA tangu nchi hii ipate uhuru. Pamoja na hayo kuna vijana wengi sana ambao wanamaliza elimu ya msingi na sekondari lakini vijana hawa wanakimbilia mijini kwa sababu hawajaandaliwa juu ya suala zima la kupata stadi za maisha. Hivyo basi, niiombe Serikali yangu tukufu kuanzisha Chuo cha VETA haraka iwezekanavyo katika Wilaya ya Lushoto ili kuwanusuru vijana wetu na kutokukimbilia mijini. Pamoja na hayo Lushoto kuna majengo ambayo yapo tayari kwani kuna karakana ya seremala na jengo kubwa la gereji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali yangu iwawezeshe hawa wakaguzi wetu wa elimu Wilayani. Watu hawa wanapata taabu sana kwa kuwa hawapati bajeti yoyote hivyo kushindwa kufanya kazi zao za kutembelea shule na hii pia inachangia kushuka sana kwa elimu. Kwa mfano, Wilaya ya Lushoto ni ya milima na mabonde, kwa hiyo, Wilaya ile inahitaji miundombinu ya magari pamoja na mafungu ya rasilimali fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya na Jimbo la Lushoto kuna shule za msingi zaidi ya 90 na seondari 35 lakini shule hizi zinakabiliwa na changamoto za walimu hasa wa masomo ya sayansi pamoja na nyumba za walimu. Pamoja na hayo walimu wetu watengenezewe mazingira mazuri pamoja na kuwapa motisha pale wanapofanya vizuri, lakini pia Serikali iboreshe miundombinu ya shule zetu kwani shule zilizo nyingi zinahitaji kukarabatiwa pamoja na kujenga matundu ya vyoo yaliyojaa, na yaliyobomoka yafanyiwe ukarabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna haya maboma yanayojengwa kwa nguvu za wananchi, niiombe Serikali yangu ipeleke nguvu ya kumalizia majengo yake, pamoja na hizi maabara nyingia ambazo zimesimama kwa sababu wananchi wamejenga mpaka mtambaa wa panya yaani (kwenye lenter) na mengine yamepigwa mpaka na bati. Niombe Serikali yangu sasa imalizie maabara hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niiombe Serikali ipeleke vitabu vya kiada na ziada kwa wakati kwani hii nayo ya kutokupeleka huduma hii kwa wakati kunasababisha kushuka kwa elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali yangu Tukufu, hili suala la chakula cha mchana ilichukue kwani wazazi walio wengi hawana uwezo na hii inasababisha wanafunzi hasa kwa wale ambao wazazi wao hawajachangia, hujisikia vibaya na kuathirika kisaikolojia, na kumsababisha mwanafunzi kutozingatia masomo anayofundishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.