Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga hoja mkono mia kwa mia. Pia nashukuru sana Mheshimiwa Waziri, Joyce Ndalichako kwa msaada mkubwa alionisaidia kwa shule ya sekondari ya Kirando kwa kunisaidia shilingi 138,000,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wanafunzi waliopewa mimba kurudi shule baada ya kujifungua haikubaliki kabisa, kwa kuwa kwanza tunapinga mimba za utotoni wakati tunasema mtoto anayestahili kuolewa ni miaka 18. Je, unahitaji sasa mtoto aolewe au azae chini ya miaka 18? Tunajikanganya na kuna sheria, mtoto anyonye kwa miaka miwili, pia tutaongeza watoto wa mitaani tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mtoto kama anaanza mapenzi angali mwanafunzi vipi achanganye masomo na mapenzi? Kwa hiyo, turuhusu hata watoto chini ya miaka 13 waolewe kwa kuwa hata akijifungua ataendelea na masomo. Tukiruhusu ni kuruhusu wanafunzi wazae na kupata UKIMWI. Naiomba Wizara ikatae kabisa suala la kuruhusu mwanafunzi aliyepewa mimba kurudi darasani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiruhusu wanafunzi wanaopata mimba warudi mashuleni tutafungulia kwa walimu wasio kuwa waaminifu kufanya mapenzi na wanafunzi na kuwasaidia kimasomo kwa mapatano ya kuishi nao kimapenzi. Mimi sikubaliani na kufanya zinaa kabla ya ndoa na kuongeza watoto wasio kuwa na baba zao na kuongeza mzigo kwa Taifa letu.