Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto nyingi sana katika mfumo wa elimu hivyo ni vyema Wizara ikajiwekea malengo mahususi (prioritise list ya issues) ambayo yanatakiwa kuwa addressed mwanzo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ubora hafifu wa ufundishaji, hakuna mfumo maalum (pedagogical skills) ambao unatumika katika kufundisha mashuleni, jambo hili linatakiwa kupewa kipaumbele cha juu kabisa kwani lina impact kubwa sana katika kuelimisha.

Katika mfumo wa sasa tunakosa walimu bora ukilinganisha na miaka ya zamani (mpaka 1990) ambapo walimu wengi walikuwa wana dedication kubwa sana katika kufundisha na kuelimisha. Walimu walikuwa na uelewa mpana wa masomo wanayoyafundisha, walikuwa na more ethics na walikuwa creative katika kuhakikisha somo lake husika linaeleweka na kupendwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna umuhimu mkubwa wa kufumua upya utaratibu wa upatikanaji wa walimu (mchujo na mafunzo), kuboresha malipo kwa walimu na mazingira rafiki ya kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mazingira duni ya kusomea wanafunzi, kuna haja kubwa ya kufanya assessment katika kila Wilaya na kwamba kila Wilaya itoe list ya shule ilizonazo katika kila Kata, hali ya shule husika na kadhalika ili kuweza kupanga mipango na utekelezaji wa mikakati husika na kuweza ku-address challenges kama matundu ya vyoo, madarasa, maabara, vitendea kazi (mazingira duni ya kujifunzia).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto ya usawa (wa kike na wasiojiweza); still ipo dhahiri hasa kwa watoto/vijana wa kike, wasiojiweza/walemevu. Mazingira ya sasa katika shule nyingi kuanzia za awali mpaka vyuoni nyingi hazina mazingira rafiki ya kuwawezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum kuweza kuhudhuria masomo au hata shughuli za practicals ama shughuli za michezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukosa falsafa ya elimu yetu, hii ipo dhahiri katika utahini, shuleni, udhibiti wa ubora wa elimu katika uandaaji wa elimu. Je, nchi yetu inasimamia katika nini? Dira ni nini? Kuna link yoyote katika mlengo wa uchumi wa kati na uchumi wa viwanda? Hii ipo reflected vipi katika education system yetu? Haya ni masuala muhimu ya kuzingatia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwajibikaji mdogo kwenye elimu, hakuna policy yoyote itakayoweza kutekelezwa bila kuwa translated kwenye bajeti. Ni muhimu kuweka bayana Wizara ya Elimu na TAMISEMI kuonesha (ku- tally) zimepanga kujenga madarasa mangapi. Zimeletwa shilingi ngapi kwa mwaka 2017/2018? Wizara ya Elimu ina mpango mkakati gani wa kumaliza tatizo la madarasa?