Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza kabisa nawapongeza Wizara ya Elimu hasa Profesa Ndalichako, Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa kazi wanayofanya. Namshukuru sana alinisaidia hata pesa kwa ajili ya high school yangu ya Kirando kwa ajili ya kujenga mabweni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitazungumzia mada moja tu kuruhusu watoto walioko shuleni kupewa mimba na kurudi kusoma. Ndugu zangu hapa Bungeni akinamama walio wengi wanaongoza mapambano mtoto asiolewe chini ya miaka 18. Leo kuna wasichana wanavunja ungo wana miaka 10 mpaka 12, wanaweza kupata mimba na mnaruhusu waende mashuleni. Mtoto yeyote anayefanya mapenzi na shule elimu yake inapungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wanithibitishie baadhi ya akinamama hapa walikuwa wanafunzi na tuko nao hapa, kama walianza mapenzi mapema huko shuleni elimu yake ilikuwaje? Wakituthibitishia walianza mapenzi bado wako shuleni na elimu yake ilikuwa pale pale mimi nitawaunga mkono, watueleze. Mimi kama Muislam, dini yangu inaniambia kabisa nisikurubie zinaa. Sasa kama Muislam anasimama hapa ana-support mtoto wa shule aanze zinaa huyo siyo Muislam, amekiuka maadili yake ya dini moja kwa moja.

TAARIFA...

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubali kabisa, naunga mkono. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwaambia ndugu zangu tusizalishe kundi la watoto wa mitaani. Watoto ambao watakuwa hawana walezi, watakuwa wazururaji hakuna atakayekubali mimba za watoto wa shule. Kwa hiyo, mnataka kuongeza watoto wa barabarani moja kwa moja, hatuwezi kukubali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wengi mpaka sasa hivi tunajua siyo waaminifu, ndiyo watafungulia sasa, wataanza kuishi na watoto wetu mashuleni, hiyo hatutakubaliana.

TAARIFA...

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza taarifa yake naikataa na huyo Shekhe aliyekwambia siyo Shekhe ni shehena. Hakuna Shekhe atakuambia tukakurubie zinaa huyo siyo Shekhe ni mnafiki wa Mashekhe! Shekhe yeyote hawezi kwenda kinyume na Quran huyo ni mnafiki wala siyo Muislam, nakwambia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusicheze na kuongeza watoto wa mitaani. Kwanza kuna UKIMWI, Sheria za Ndoa siku hizi kwa Mapadri na Mashekhe huolewi mpaka upimwe UKIMWI ndiyo ndoa inafungwa. Leo utashirikishaje watoto wafanye zinaa shuleni hawapimwi UKIMWI. Ndugu zangu tusikubaliane, mimi napinga hoja zenu, mmekaa wanawake mnataka kutuendesha, mwisho mtaruhusu ndoa za jinsia moja au ndoa za kusagana hapa, acheni.

Nithibitishie wewe kama kweli ulianza mapenzi bado uko mwanafunzi. Tuelezeni kati yetu nani alianza mapenzi bado mwanafunzi? Nashaanga Mwalimu mmoja anasimama hapa anasema turuhusu mimba, hao Walimu wa namna hiyo ndiyo siyo waaminifu. Inawezekana waliwapa watoto wetu mimba tuwachunguze, tuwachukulie hatua huko walikokuwa wanafundisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana walikuwa wanaishi kimapenzi na wanafunzi. Ni makosa kabisa kuishi na mwanafunzi na makosa kabisa kutembea na mtoto chini ya miaka 18. Mtu aliyebaka kifungo chake ni miaka 30, tuache sheria ichukue mkondo wake lakini hatuwezi kuruhusu sisi kuwaozesha watoto wako shuleni.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila mpangilio)

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ndiyo hiyo, ahsante sana na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja