Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia mchana huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, naomba nichukue fursa hii kwanza kumpongeza Waziri na Naibu Waziri wa Elimu. Kwa kweli Mheshimiwa Waziri amekuwa msikivu, mkarimu, akipigiwa simu anapokea na tukimpelekea matatizo yetu ya elimu anatusikiliza kwa utii na uadilifu mkubwa. Nimwombee kwa Mwenyezi Mungu aendelee kuwa na hilo hilo sikio la usikivu, liambatane vilevile na kusikia hoja ambazo tunaziwasilisha tunapochangia bajeti yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walatini wana msemo, non scholae sed vitae discimus, wakimaanisha we do not learn for school but we learn for life. Mfumo wetu wa elimu lazima utambue kwamba tunatengeneza maisha yetu, maisha ya watoto wetu, maisha ya wajukuu zetu na maisha ya kizazi kijacho. Mjadala unaoendelea ni uthibitisho tosha tumejikwaa kwenye kutengeneza kizazi chenye matumaini ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapopata vitabu vinavyokinzana, tunapopata mifumo ya elimu inayotofautiana kwenye Taifa lilelile, inayonung’unikiwa upande mmoja na upande mwingine ni tafsiri tosha Mheshimiwa Waziri ana kazi kubwa ya kufanya kwenye hili. Nimwombe hoja zinazohusu hadhi, value, quality ya elimu yetu, azibebe vizuri na azifanyie kazi kwelikweli, tukifanya hivi tutatengeneza Taifa ambalo lina matumaini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na mifumo mizuri sana siku za nyuma na wote tumepitia kwenye mifumo. Mkono wa kulia na wa kushoto haufanani. Hata huohuo mkono wa kulia una vidole vitano vyenye urefu tofauti na Mwenyezi Mungu katuumba hivyohivyo tulivyotofautiana na yeye ana makusudi ili tutegemeane. Haiwezekani wanafunzi wote Tanzania nzima wakawa na upeo sawa, wakawa na fikra sawa, wakaenda sawasawa. Ndiyo kuna watu ambao Mwenyezi Mungu kawaumba wanafaa kuwa wanasayansi, madaktari, watu wa art, watu wa kilimo na wengine watu wa biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii iko wapi SHYCOM? Mtu toka akiwa mtoto mdogo anajua akipenda biashara basi kuna form five na form six iko SHYCOM. Ziko wapi zile Shule za Ufundi za Ifunda, Mbeya Tech, Dar Tech, Arusha Tech ziko wapi leo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo tunapokwenda kusema tunatoa elimu za ugoko, tusiangalie tulikodondokea tuangalie pale tulipojikwaa. Nimwombe Waziri, hata mnaposema university sijui zote ziko sawa, mimi namwambia hakuna kitu kama hicho, ni kanuni ya maisha. University ya Mzumbe lazima itakuwa tofauti na University ya Tumaini kwa hoja za kihistoria, kwa hoja za infrastructure, kwa hoja ya curriculum, kwa hoja zote utakazotaka kuziweka. Mimi nimwombeni sana, hili jambo ni lazima tuliweke vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine kukaririshwa madarasa. Hili wala hatuhitaji kuweka utaratibu kwamba watu wote wapite kutoka darasa la kwanza mpaka la saba bila kukaririshwa darasa, sasa kuna haja gani ya kufanya mitihani na mitihani tunafanya kwa ajili ya nini? Mitihani hii imewekwa kwa ajili ya ku-control human behavior. Usipopata tishio huwezi ukafanya au uka-behave, it is human nature.

Mheshimiwa Mwenyekiti, human nature siku zote jinsi ilivyo lazima umwekee utaratibu wa kumfanya akae kwenye mstari. Moja kati ya vitu hivi ni pamoja na kuweka mitihani, lingine usipofikisha wastani tutakufukuza, ni kama tulivyoweka sheria na taratibu nyingine. Sasa huku mnasema waende tu kwa nini mkifika university kuna ku-carry over, kuna supplementary, this is contradiction! Tunaji-contradict sisi wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukisema hii elimu tunaiburuzaburuza, sawa twendeni lakini mimi niwaambieni kama university mnasema kuna ku-supp, tafsiri yake ni kwamba tunataka tutengeneze a certain quality of education, the same i-apply kwenye ngazi zote. Walatini wanasema, repetitio est mater studiorum…

Mambo uliyoyafanya toka ukiwa darasa la kwanza ndiyo yanayokujenga wewe mpaka unapokuwa university. Sasa huku aende holela halafu akifika university ndiyo kwanza apate utaratibu, haya mambo hayawezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme lingine, hili naomba niseme kwa utaratibu kidogo, ni jambo ambalo limegusa hisia nyingi sana za watu, ni suala la mimba za utotoni, mimba za shuleni, yule anayepata mimba aendelee na mafunzo au arudi akajifungue na atafutiwe utaratibu mwingine wa masomo. The same spirit tunayoiweka kwenye kuitengeneza elimu ya nchi yetu izingatie mila na desturi, izingatie taratibu lakini vilevile izingatie mazingira mazuri yanayofanya kitu kinachoitwa social structure vis-a-vis social responsibilities, maana yake nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamii yetu hii imekaa katika makundi ya rika, tunatarajia mtoto wa darasa la kwanza mpaka darasa la saba atakuwa na behavior fulani inayoendana na jamii. Atakayekwenda university ata-behave tofauti na atakayetoka hapa akawa baba, mfanyakazi, mzee mpaka kikongwe, hiyo ni social structure imetengenezwa. Mwenyezi Mungu ameumba kuna muda wewe utasoma, kuna muda utapevuka utazaa, kuna muda utakuwa baba, kuna muda utakuwa kiongozi, kuna muda utakuwa mzee umezeeka baadaye una-rest in peace.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongea juzi, nashukuru waliosema hapa wengi tulikuwepo, wa kwanza Mheshimiwa Mama Sitta alikuwepo, wa pili Mheshimiwa Susan Lyimo alikuwepo, Mheshimiwa Ndassa alikuwepo, tuliongelea kuhusu wale watoto wa Shinyanga waliopata mimba wakiwa watoto, tulilia na kusikitika. Tukajipanga kule tukasema tuje hapa Bungeni tushinikize Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 ambayo inaruhusu mtoto wa kike aolewe akiwa na miaka 14 tuifute.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunataka watoto wazae warudi shuleni. Tunajichanganya wenyewe hatujui tunakotaka kwenda. Leo hii tuna ajenda kubwa sana ya kuhakikisha Sheria ya Ndoa inayomkandamiza mwanamke tuiondoe halafu huku wazae, hivi sisi tumelogwa, hatujui tunachokitaka. Basi niwaulize swali moja, kama tunaruhusu mimba mashuleni, kuna mechanism gani ambayo tumeiandaa kuhakikisha kwamba hawa watoto hawataoana mashuleni? This is a contradiction! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe mama zangu na mimi natokana na mama, naelewa…

TAARIFA...

HE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Ndiyo hapo unapopata tofauti kati ya kuelimika na elimu. Ukipata tofauti kati ya kuelimika na elimu hutapata shida. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani unaposema huyu mtu asiolewe akiwa chini ya miaka 18, tafsiri yake nini? Hata Sheria ya Ndoa wanakuambia ndoa haiwezi ikawa ndoa mpaka mke na mume waingiliane. Tafsiri yake kama wanaingiliana maana yake kuna mimba. Yaani vitu vingine jamani wala hatuhitaji kutafuta misamiati, hatuhitaji kutafuta maneno ya kupakana matope.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalize na neno moja, naomba nilinde kwenye muda wangu. Najua hili jambo lina hisia, hasa kwa mama zetu hata kama mimi ningekuwa mama nisingependa mwanangu limkute baya. Kihistoria sisi tuliotoka kwa mama zetu tuna mapenzi ya dhati sana kati ya mama na mtoto, mama siku zote hupenda mwanaye yasimkute mabaya. Katika upendo huu wa mama kumpenda mwanae kuna maeneo upendo humletea madhara mtoto.

TAARIFA...

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Na iwe kama ulivyonena nani amewaroga. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hali ya kawaida niwaombe sana jambo hili tulitazame katika mapana, ni jambo lililogusa hisia, hakuna mstari ulio-clear unaoweza kutofautisha mimba ya mtoto anayepata chini ya miaka18 na ndoa. Tukihalalisha hilo basi tukubaliane kimsingi tunataka ile Sheria ya mwaka 1971 iendelee kuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.