Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii, na mimi naomba kidogo nichangie kwenye Wizara hii ya Elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kwenye suala la elimu bure ama elimu bila malipo. Sera hii ni sera nzuri kwa maana ya kuwasaidia Watanzania wengi ambao watoto wao walikuwa hawajaandikishwa mashuleni, kama Kambi ya Upinzani ilivyotoa hotuba yake ni hii ni sera inayohitaji tathmini ya hali ya juu ili kuwa na manufaa katika Taifa, vinginevyo inaweza ikawa ni sera yenye matatizo ambayo baadae tutakuja hapa Bungeni kuanza kusutana wenyewe kwa wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninafikiri kwamba ni lazima tuangalie namna gani tunapokea mapendekezo ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, kuangalia miundombinu ya elimu yetu, kuangalia majengo yetu ya utawala, kuangalia ikama ya walimu wetu katika kuhakikisha kwamba watoto

wanaoandikishwa wanapata elimu bora. Shida ya mfumo huu ni kwamba sasa unasababisha elimu iwe katika ubora wa hali ya chini sana na lengo siyo kuwa na mfumo ambao utaturudisha katika elimu ambayo haina ushindani. Ni lazima kuwe na ushindani kati ya elimu inayotolewa na private school na elimu inayotolewa na shule zetu za umma. Sasa ushindani huo haupo kwa sasa. Kwa upande wa shule zetu za umma na shule za private bado dhana si kuwasaidia wazazi wapeleke watoto wao katika shule za umma, dhana inawafanya wazazi sasa wapeleke watoto katika shule za private. Kwa hiyo, wasio na uwezo bado hawasaidiwi katika huu mfumo tulionao. Ni vizuri sana tuangalie huu mfumo kwa upana wake wa kutosha ili uwe na faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uelewa wangu hata huko nyuma kinachoendelea sasa kilikuwa kinafanyika, kwa sababu kilichoondolewa hapa kwa upande shule za msingi ni ada ya kuandikisha wanafunzi shuleni ambayo ndiyo ilikuwa kikwazo. Kwa mfano, sekondari ni ada ya shilingi 20,000 ama 70,000 lakini kwa upande wa tuition ilikuwa inabebwa na Serikali mlichokitangaza ni kuondoa michango ambayo wazazi walikuwa tayari wanalipa matokeo, yake wazazi wameamua ku-relax hawataki kulipia michango watoto wao. Sasa hivi mmezilazimisha Halmashauri zianze kukamata wazazi na kuwapeleka polisi kuanza kuwafungulia kesi na bahati mbaya kwa sababu hamkuwa na transitional period, hamkujiandaa vizuri namna gani baada ya kutangaza huu utaratibu mtahakikisha kwamba ni namna gani Halmashauri zinawabana wazazi, sasa wanatumia Sheria ya Ustawi wa Jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kw ahiyo ni rai yangu kwako Mheshimiwa Waziri, kwa sababu ni sera, zielekezeni Halmashauri zianzishe by-laws ambayo itawalazimisha wazazi waweze kulipia watoto wao na kama hawawalipii waweze kuadhibiwa kwa Sheria za Halmashauri zisizozidi shilingi 50,000 kuliko sasa kuwapeleka Polisi unnecessarily. Kwa hiyo nilikuwa nafikiri ni jambo la msingi sana kuliangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie habari ya maslahi ya walimu. Kwanza walimu wana madeni mengi wanaidai Serikali kama Kambi ya Upinzani ilivyoonesha, ambapo bado kuna zaidi ya shilingi bilioni 138 wanadai hawajalipwa. Hiyo inaondoa moral yao ya kutimiza wajibu wao wa kuelimisha watoto wetu, hivi hapa katika Serikali ambayo ina miaka zaidi ya 55 bado tunapaswa ku-debate habari ya maslahi ya walimu ya madeni yao badala ya kufikiri kwamba ualimu ingetakiwa iwe ni rear professional ambayo tunatakiwa watu watu wanaokuwa Walimu tuwalipe vizuri. Leo ualimu umekuwa kama ni ile ajira ambayo inatupiwa watu walioshindwa ndiyo mtu anakuwa mwalimu, haiwezekani! Hatuwezi kulea Taifa ambalo wanaopaswa kuelimisha watoto wetu ndiyo tunaifanya ni professional ya mwisho kabisa, mtu akipata division four ndiyo anakuwa mwalimu. Division zero aliyefeli ndiyo anakuwa mwalimu lazima tubadilishe huu mtazamo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunataka kuwa na elimu bora lazima tutenge maslahi ya kutosha kwa walimu. Kwahiyo nilikuwa nadhani……….

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.